Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.
Mabadiliko ya Tabianchi
UN tuondoleeni vikwazo vya silaha - Rais Salva Kiir
Rais wa Sudan Kusini, Salvar Kiir Magardit, ametaka nchi yake kuondolewa vikwazo vya silaha akieleza vinakwamisha maendeleo ya nchi yao.
Tunaelimisha wanafunzi na vijana kuhusu mabadiliko ya tabianchi - Madina Jubilate Kimaro
Wiki hii hapa kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa kumefanyika mkutano wa tathmini ya malengo ya maendeleo endelevu SDGs kuona wapi nchi wanachama, kampuni, watu binafsi wamefikia kusongesha maendeleo hayo yanayofikia ukomo mwka 2030. Vijana nao walikuwa na siku zao mbili za kuelezea wanafanya nini kule waliko na wanataka nini kifanyike kusongesha malengo hayo likiwemo namba 13 la tabianchi. Miongoni mwa vijana walioshiriki ni Madina Jubilate Kimaro, Balozi wa Mazingira wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto duniani, UNICEF nchini Tanzania.
Muungano wa mabadiliko ya tabianchi wadai hatua, huku Guterres akionya Ubinadamu umefungua milango ya kuzimu
"Joto la kupindukia linaleta madhara ya kutisha duniani ", kwa mujibu wa mkuu huyo wa Umoja wa Mataifa akizungumza leo katika mkutano wa kwanza kabisa wa ngazi ya juu wa matarajio kuhusu mabadiliko ya tabianchi mbele ya mbele ya muungano wa kimataifa wa kuchagiza hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi ulijumuisha wachagizaji, watendaji, wanasiasa, wafanyabiashara, mashirika ya kimataifa na viongozi wa asasi za kiraia waliokusanyika New York kandoni mwa mjadala wa Baraza kuu UNGA78.
Mradi wa ufugaji wa Samaki umenikombia mimi na familia yangu: Michael Chiwayi
Mkutano wa ngazi ya juu kuhusu mabadiliko ya tabianchi unafanyika leo kwenye makao Makuu ya Umoja wa Mataifa kandoni mwa mjadala mkuu wa Baraza Kuu , UNGA78 lengo likiwa kuzihamasisha nchi wanachana kuchukua hatua zaidi kuzinusuru nchi zinazobeba mzigo mkubwa wa athari za janga hilo.
Sasa ni wakati wa kulitoa azimio la SDGs kwenye karatasi na kulitekeleza kwa vitendo:UN
Jukwaa la ngazi ya juu la kisiasa kuhusu malengo ya maendeleo endelevu SDGs limefunga pazia jioni hii kwenye makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York kwa kupititishwa azimio la kisiasa la kusongesha mchakato wa kufikia malengo hayo.
Jiungeni na EAC tupate nguvu zaidi ya kuweza kuwasaidia
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Dkt. Peter Mathuki amezisihi nchi nyingi zaidi zilizopo katika ukanda huo kujiunga na jumuiya yao ili waweze kuwa na nguvu zaidi na pale zitakapokumbwa na changamoto waweze kuwasaidia kwa karibu zaidi kama jumuiya.
Tunakumbatia wito wa kupambana na mabadiliko ya tabianchi kwa vitendo - Vijana Bongoyo Tanzania
Wakati macho na masikio ya Dunia yakielekezwa hapa New York Marekani kwenye mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa utakaoanza Jumatatu wiki ijayo kujadili mada mbalimbali ikiwemo hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi , tunaelekea Tanzania ambako katika pitapita zake, Flora Nducha alipokuwa jijini Dar es Salaama alikutana na mmoja wa vijana wajasiriamali kwenye kisiwa cha Bongoyo waliokumbatia wito wa kupambana na jinamizi la mabadiliko ya tabianchi, akamweleza Flora kuwa mbali ya kujipatia kipato kutokana na utalii endelevu ana jukumu kubwa pamoja na baadhi ya vijana wenzie la kul
Kutochukua hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi kunaweka rehani maisha ya watu: WMO
Ukosefu wa hatua za kutosha kuelekea utimizaji wa malengo ya mabadiliko ya tabianchi unapunguza kasi ya mapambano ya kimataifa dhidi ya umaskini, njaa na magonjwa hatari, kulingana na ripoti iliyotolewa leo na shirika la hali ya hewa la Umoja wa Mataifa WMO.
Takriban watu 3, 000 wamekufa na 10,000 hawajulikani waliko kufuatia mafuriko Libya:WMO/WHO/IOM/IFRC
Mafuriko makubwa yaliyoikumba Libya tarehe 10 September yamesababisha maafa ikiwemo vifo vya takriban watu 3,000 na wengine zaidi ya 10,000 kutojulikana waliko Mashariki mwa nchi hiyo kwa mujibu wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na shirikisho la kimataifa la chama cha msalaba mwekundu IFRC na mwezi mwekundu.
Dola Bil 360 zinahitajika kwa mwaka ili kufikia usawa wa kijinsia 2030
Takwimu mpya zilizokusanywa na mashirika mawili ya Umoja wa Mataifa zimeonesha kuwa kuna haja ya uwekezaji wa ziada wa dola bilioni 360 kwa mwaka ili kufikia usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa wanawake ifikapo 2030.