DR Congo: Wanajeshi wa kulinda amani watumwa kulinda raia huko Ituri
Wanajeshi wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa wamekuwa wakikabiliana na machafuko mapya dhidi ya raia Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo DRC, wakishika doria na kuwasaidia viongozi wa eneo hilo kuwaachilia huru watu watano waliotekwa nyara na wanamgambo katika jimbo la Ituri.