Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

DR Congo

Bi. Keita akizungumza na wanahabari huko Kalehe, Kivu Kusini.
MONUSCO/Michael Ali

MONUSCO yaafikiana na serikali ya DRC mikakati ya kuondoka nchini humo

Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC na Mkuu wa wa mpango wa Umoja wa Mataifa nchini humo MONUSC, Bi Bintou Keita na Naibu Waziri Mkuu, na Waziri wa Mambo ya nje Francophonie Christophe Lutundula walithibitisha jana Jumamosi Januari 13, dhamira ya vyombo hivyo viwili kufanya kazi kwa pamoja kwa mchakato wa kuondoka kwa MONUSCO nchini DRC kwa njia ya maendeleo, kuwajibika, heshima na kwa MONUSCO kuwa mfano wa kuigwa. 

Julienne Lusenge, mwanaharakati wa haki za binadamu wa Kongo ambaye ni rais wa kundi la Sofepadi na mkurugenzi wa Mfuko wa Wanawake wa Kongo wakati wa mkutano na waandishi wa habari kuhusu unyanyasaji dhidi ya wanawake katika migogoro. (Maktaba - 25 Febr…
UN Photo/ Jean Marc Ferré

Mahojiano: SOFEPADI ilivyomsaidia manusura wa ukatili wa kingono Ituri, nchini DRC

Ukatili wa kingono vitani ni jambo linalokumba wanawake, na wasichana Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC. Wanapobakwa na kupewa  ujauzito wengi wao hukosa pa kukimbilia kusaka msaada wa kiafya na kisaikolojia. Julienne Lusenge, mshindi wa tuzo ya Umoja wa Mataifa ya haki za binadamu kwa mwaka 2023 kwa kutambua hilo mwaka 2000 aliunda SOFEPADI, shirika la kiraia la kusaidia wanawake na watoto waliokumbwa na ukatili wa kingono na ubakaji. 

Mtoto akiwa katika kambi ya wakimizi wa ndanijimboni Ituri nchini DRC  kufuatia kufurushwa makwao kutkana na mapigano mashariki mwa nchi
© UNICEF/Diana Zeyneb Alhindawi

Kikosi cha kwanza cha SADC chawasili DRC kusaidia kukabili mapigano mashariki mwa nchi

Huko nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, wanajeshi wa kikosi cha kwanza kutoka Jumuiya ya Maendeleo ya nchi za kusini mwa Afrika, SADC kitakachokuwa na jukumu la kusaidiana na jeshi la serikali, FARDC kujibu mashambulizi kutoka kwa vikundi vilivyojihami mashariki mwa nchi hiyo, wamewasili huko Goma, mji mkuu wa jimbo la Kivu Kaskazini.

Sauti
1'37"
Bendera ya Umoja wa Mataifa ikikabidhiwa kwa maafisa wa MONUSCO nchini DRC kuashiria kufungwa kwa ofisi ndogo za ujumbe huo wa Umoja wa Mataifa wa Kulinda amani kwenye eneo hilo lililoko kilometa takribani 140 kutoka mji wa Beni jimboni Kivu Kaskazini.
UN/George Musubao

Ofisi ya MONUSCO Lubero, Kivu Kaskazini yafungwa

DRC, MONUSCO umefunga kituo chake kilichoko Lubero jimboni Kivu Kaskazini baada ya kuweko huko kwa miaka 21.Hatua hii ni sehemu ya utekelezaji wa mpango wake wa kujiondoa kwa utaratibu kutoka DRC, kwa mujibu wa azimio la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kufuatia ombi la serikali ya DRC.

Bukavu, Kivu Kusini. Uchaguzi wa Rais na wabunge umefanyika katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, 20 Desemba 2023.
MONUSCO/Michael Ali

DRC: Maisha yarejea hali ya kawaida huko Fataki, Ituri baada ya mashambulizi kutoka CODECO

Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kazi ya kuhesabu kura inaendelea baada ya uchaguzi mkuu uliofanyika Jumatano na kuendelea katika baadhi ya maeneo jana Alhamisi, huku ikielezwa kwamba jimboni Ituri, maisha  yamerejea katika hali ya kawaida kwenye eneo la Fataki baada ya mwaka mmoja wa mashambulizi kutoka kwa wanamgambo waliojihami wa kundi la CODECO. 

Sauti
1'20"
Upigaji kura wa kuchagua Rais na Wabunge huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC. Hapa ni Bukavu jimboni Kivu Kusini 20 Desemba 2023
MONUSCO Michael Ali

Uchaguzi DRC: Matokeo ya awali yaanza kubandikwa, wengine walipiga kura leo

Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, matokeo ya awali ya uchaguzi mkuu wa rais, magavana, wabunge na madiwani ambao ulifanyika jana, yameanza kubandikwa katika baadhi ya vituo huku maeneo mengine wapiga kura ambao  hawakuweza kupiga kura kutokana na sababu mbali mbali ikiwemo mvua na kuchelewa kuwasili kwa vifaa wameruhusiwa kupiga kura yao leo Alhamisi.