Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

DR Congo

Innoss B(kushoto) na Mkurugenzi wa WFP DRC, Peter Musoko(Kulia). Innoss B akitia saini barua rasmi ya kuteuliwa kama Msaidizi wa Ngazi ya Juu wa WFP nchini DRC, akihimiza milo yenye afya na lishe bora.
© WFP/Charly Kasereka

Innoss’B kutumia muziki kusongesha elimu na lishe bora DRC

Nimeshuhudia njaa mara nyingi sana wakati wa utoto wangu, kabla ya kwenda shule tulikuwa na njaa na kabla ya kulala tulikuwa na njaa, ndivyo asemavyo mwanamuziki Innocent Balume, al maaruf Innoss’B ambaye ametangazwa kuwa muungaji mkono wa ngazi ya juu wa shirika la  Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula duniani, WFP katika kusongesha milo yenye afya na lishe bora nchini mwake Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Sauti
2'6"
Ugawaji wa dharura wa chakula unaendelea Mashariki mwa DRC. (Maktaba)
© WFP/Michael Castofas

WFP: kuna uhaba wa chakula mashariki mwa DRC

Umoja wa Mataifa unasema wananchi milioni 23.4 sawa na robo ya wananchi wote takriban milioni 96 wa Jamhuri ya Kidemokrasia Kongo DRC, wanakabiliwa na njaa. Wengi wa wananchi hao wanaishi katika hali duni na yenye msongamano wa watu wasio na uwezo wa kupata chakula, huduma za afya na elimu.

Helikopta za MONUSCO zikizunguka Ituri DRC (Kutoka Maktaba)
MONUSCO/Nazar Voloshyn

Shambulizi dhidi ya walinda amani DRC, UN yalaani

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amelaani shambulizi ambalo limetokea jana Jumamosi Machi 16 na kujeruhi wanajeshi wanane wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, wakati wa mapigano kati ya waasi wenye nguvu wa M23 na wanajeshi wa Serikali.

Kamanda wa TANZBATT-10, Luteni Kanali John Peter Kalabaka akimkabidhi bendera ya Tanzania Luteni Kanali  Vedasto Ernest Kikoti ikiwa ni ishara ya kukabidhiana majukumu ya ulinzi wa amani huko Beni Mavivi jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokra…
TANZBATT-10

Wananchi DRC eleweni na ikubalini dhamira ya UN ya kulinda raia - TANZBATT-11

Hii leo huko jimboni Kivu Kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, kikosi cha 10 cha Tanzania (TANZBATT-10)  kilichoko kwenye brigedi ya mapigano (FIB) ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO imekabidhi majukumu kwa kikosi cha 11, TANZBATT-11, katika hafla iliyofanyika eneo la Beni-Mavivi. Msimulizi wetu ni Kapteni Abubakari Muna, Afisa Habari wa TANZBATT-10.

Sauti
3'28"
Wanawake katika kijiji cha Doi DR Congo
UN Photo/Martine Perret

Wanawake na wasichana ni ufunguo wa mustakbali wa DRC: WFP

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP yupo ziarani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC ambapo katika kuelekea siku ya wanawake duniani itakayoadhimishwa Ijumaa Machi 8 wiki hii ametembelea vikundi vya wanawake wajasiriamali wanaojishughulisha na shughuli mbalimbali za kuwaingizia kipato .