Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

DR Congo

Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa na wa Misaada ya Kibinadamu Bruno Lemarquis alipozuru DRCongo mapema Machi
© UNOCHA

Pande zinazozozana mashariki mwa DRC zakumbushwa wajibu wa kulinda raia

Mratibu wa Misaada ya Kibinadamu wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, Bruno Lemarquis, ameonesha wasiwasi mkubwa kuhusu ghasia zinazoongezeka katika mji wa Mweso, ulioko takribani kilomita 100 kutoka Goma, katika jimbo la Kivu Kaskazini (mashariki mwa DRC), Msemaji wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amewaeleza Waandishi wa habari jijini, New York Marekani.

Wakazi wa kambi ya wakimbizi wa ndani ya Bulengo jimboni Kivu Kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC wakiwa kwenye tamasha la mpira wa soka lililoandaliwa na Shirikisho la Soka barani Afrika, na kufanikishwa na WFP.
© WFP/Michael Castofas

Afcon: Shamrashamra zagubikwa na ukimbizi na njaa mashariki mwa DRC

Huko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC shamrashamra za mashindano ya Kombe la Mataifa Afrika, Afcon yanayoendelea huku Côte d'Ivoire zinagubikwa na ukimbizi na ongezeko la matukio ya ukatili wa kingono huku shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula duniani, WFP likichukua maamuzi magumu kutokana na ukata unaokabili operesheni zake. 

 

Bi. Keita akizungumza na wanahabari huko Kalehe, Kivu Kusini.
MONUSCO/Michael Ali

MONUSCO yaafikiana na serikali ya DRC mikakati ya kuondoka nchini humo

Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC na Mkuu wa wa mpango wa Umoja wa Mataifa nchini humo MONUSC, Bi Bintou Keita na Naibu Waziri Mkuu, na Waziri wa Mambo ya nje Francophonie Christophe Lutundula walithibitisha jana Jumamosi Januari 13, dhamira ya vyombo hivyo viwili kufanya kazi kwa pamoja kwa mchakato wa kuondoka kwa MONUSCO nchini DRC kwa njia ya maendeleo, kuwajibika, heshima na kwa MONUSCO kuwa mfano wa kuigwa. 

Julienne Lusenge, mwanaharakati wa haki za binadamu wa Kongo ambaye ni rais wa kundi la Sofepadi na mkurugenzi wa Mfuko wa Wanawake wa Kongo wakati wa mkutano na waandishi wa habari kuhusu unyanyasaji dhidi ya wanawake katika migogoro. (Maktaba - 25 Febr…
UN Photo/ Jean Marc Ferré

Mahojiano: SOFEPADI ilivyomsaidia manusura wa ukatili wa kingono Ituri, nchini DRC

Ukatili wa kingono vitani ni jambo linalokumba wanawake, na wasichana Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC. Wanapobakwa na kupewa  ujauzito wengi wao hukosa pa kukimbilia kusaka msaada wa kiafya na kisaikolojia. Julienne Lusenge, mshindi wa tuzo ya Umoja wa Mataifa ya haki za binadamu kwa mwaka 2023 kwa kutambua hilo mwaka 2000 aliunda SOFEPADI, shirika la kiraia la kusaidia wanawake na watoto waliokumbwa na ukatili wa kingono na ubakaji.