Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

DR Congo

Bintou Keita kutoka Guinea, ni Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa UN nchini DRC na Mkuu pia wa MONUSCO
N /Eskinder Debebe

Taarifa nyingi mbaya kuhusu MONUSCO ni upotoshaji: Bintou Keita

Mwakilishi wa katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC , Bintou Keita amefanya Mkutano na mjadala na wawakilishi wa wanafunzi wa vyuo vikuu nchini humo katika mji mkuu kishasa ili kujadili suala la usalama pamoja na kupambana na usambazaji wa habari za uongo dhidi ya vikosi vya kulinda amani vya umoja wa mataifa nchini DRC, MONUSCO.

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ( Maktaba)
UN photo /Loey Felipe

Baraza la Usalama la UN lakutana kujadili DRC

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa leo Alhamisi limekuwa na kikao cha faragha kuhusu hali ya usalama nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kufuatia matukio kadhaa ikiwemo lile la jumapili iliyopita ambapo walinda amani wa ujumbe wa Umoja huo huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC MONUSCO kuua raia na kujeruhi wengine kwenye eneo la Kasindi jimboni Kivu Kaskazini mpakani na Uganda.