Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

DR Congo

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ( Maktaba)
UN photo /Loey Felipe

Baraza la Usalama la UN lakutana kujadili DRC

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa leo Alhamisi limekuwa na kikao cha faragha kuhusu hali ya usalama nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kufuatia matukio kadhaa ikiwemo lile la jumapili iliyopita ambapo walinda amani wa ujumbe wa Umoja huo huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC MONUSCO kuua raia na kujeruhi wengine kwenye eneo la Kasindi jimboni Kivu Kaskazini mpakani na Uganda.