Sanaa ya uchoraji yaepusha vijana na uhalifu huku ikipendezesha Goma
Huko Goma, mji mkuu wa jimbo la Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, wasanii vijana wanatumia sanaa ya upakaji kuta rangi kama njia mojawapo ya kuhamasisha jamii kuachana na ghasia sambamba na kueneza kauli za chuki.