Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

DR Congo

Walinda amani wa Umoja wa Mataifa wakisindikiza wapiganaji wa M23 waliojisalimisha Kivu Kaskazini.
MONUSCO

DRC: Hali ya kawaida imerejea lakini bado tete

Kaimu Mkuu wa ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC Kassim Diagne amezungumza na waandishi wa habari kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa kwa njia ya video kutoka mji mkuu Kinshasa na kusema hali ya kawaida angalau imerejea lakini bado ni tete baada ya mamlaka kutoa wito kwa waandamanaji kusitisha vitendo hivyo sambamba na jeshi la serikali, FARDC kuimarisha usalama.

Naibu Mwakilisih wa Katibu Mkuu wa UN nchini DRC Kassim Diagne akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari 26 Julai 2022, mkutano  ulihudhuriwa pia na Msemaji wa Serikali ambaye pia ni Waziri wa Habari Patrick Muyaya.
UN/Boybe Malenga

Vurugu dhidi ya ofisi za UN DRC: Serikali kuwasaka na kuwafikisha mbele ya sheria watuhumiwa

Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC imesihi utulivu miongoni mwa wananchi baada ya maandamano na uvamizi dhidi ya vituo vya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani MONUSCO kwenye miji ya Goma na Butembo jimboni Kivu Kaskazini, tukio ambalo hata Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametaka mamlaka zichunguze na sheria ichukue mkondo wake. Mwandishi wetu wa DRC Byobe Malenga ana taarifa zaidi.

Sauti
3'22"
Mfanyabiashara barabarani akiuza chakula barani Afrika
IMF

Dunia kushuhudia kudorora zaidi kwa uchumi: IMF

Ripoti ya hali ya uchumi kwa robo ya pili ya mwaka huu wa 2022 ambao ni mwezi Aprili hadi Juni ambayo imetolewa na Shirika la Fedha la Kimataifa IMF imesema matarajio ya ukuaji wa uchumi duniani yanazidi kukumbwa na kiza na yanakosa uhakika na kwamba matumaini ya uchumi kukwamuka mwaka 2021 yanazidi kuyoyoma mwaka huu wa 2022. 

Sauti
2'34"
Magari haya ya kivita ya kubeba askari wa Tanzania huko DR Congo.
TANZBATT 7/Ibrahim Mayambua

Uvamizi wa vituo vya UN DRC; Walinda amani 3 wauawa

Huko nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC mlinda amani askari wa kulinda amani na polisi  wawili wa Umoja wa Mataifa wameuawa baada ya waandamanaji kuvamia kituo cha ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo MONUSCO huko Butembo na kupora silaha za polisi wa kitaifa na kuanza mashambulizi.

Angela N'Habimana mwenye umri wa miaka 67 akiwa na mjukuu wake aitwaye Réponse kwenye kituo cha kijamii cha Kiwanja katika eneo la Rutshuru jimboni Kivu Kaskazini nchini DRC baada ya kukimbia mashambulizi kwenye makazi yao.
© UNHCR/Sanne Biesmans

Zaidi ya watu 800 wameuawa Mashariki mwa DRC kati ya Februari na Juni 2022- UNHCR

Hali ya usalama huko Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC inaendelea kuzorota ambapo shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR, linasema mauaji na uporaji wa mali za raia vinaendelea na kwamba kati ya mwezi Februari na mwezi uliopita wa Juni zaidi ya watu 800 wameuawa katika mashambulizi kutoka vikundi vilivyojihami.

Esperance Tabisha ajulikanaye pia kama Esperanza akiwa nje ya makazi yao mapya huko Ontario Canada na ni kutokana na programu ya mkimbizi kuhamia nchi ya tatu chini ya mkataba wa kimataifa wa wakimbizi wa mwaka 2018.
UN News Video

Esperance Tabisha: Kutoka kuwa mkimbizi Kakuma hadi mbunifu wa mitindo Canada

Esperance Tabisha, raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambaye sasa ni mnufaika wa mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu wakimbizi, GCR uliopitishwa mwaka 2018 wenye vipengele kadhaa ikiwemo kuhamishia wakimbizi nchi ya tatu. Alikimbia vita DRC na kuingia kambi ya Kakuma nchini Kenya mwaka 2010 na mwaka 2019 akahamia Canada kupitia msaada wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR.

Charline (kushoto) mwenye umri wa miaka 11 amekimbia mapigano huko Bunagana jimboni Kivu Kaskazini nchini DRC na kukimbilia eneo la Rutshuru yeye na familia yake. (Maktaba)
©UNICEF/Jean-Claude Wenga

Mapigano nchini DRC yanaathiri raia :UNHCR

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR limeendelea kutoa wito wa sitisho la mashambulizi dhidi ya raia jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambako matukio hayo yameendelea kusababisha vifo miongoni mwa raia.