Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au coronavirus">COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

Hitaji la dharura kuboresha mifumo ya udhibiti wa taka laonekana baada ya taka zilizotokana na kudhibiti COVID-19 kuwa tishio

Shirika la Umoja wa Mataifa la afya duniani, WHO limetoa ripoti mpya inayoonesha kuwa mifumo ya usimamizi wa taka za afya duniani kote hivi sasa imezidiwa uwezo kutokana na maelfu ya tani za taka zinazotokana na vifaa vilivyotengenezwa kwa ajili ya kukabiliana na janga la COVID-19 na hivyo kutishia afya ya binadamu na mazingira na wakati huo huo kufichua hitaji kubwa la kuboresha udhibiti wa taka zinazozalishwa kutokana na huduma ya tiba.  

Sauti
2'44"
Kisanduku cheupe cha sindano ya GSK ya Sotrovimab na chupa inayolingana ya dozi moja, iliyoonyeshwa kwenye mandharinyuma isiyo na dozi.
© GlaxoSmithKline

WHO yapendekeza dawa mbili mpya za kutibu wagonjwa wa COVID-19

Kundi la wataalamu wa miongozo wa WHO wametaja dawa ya Baricitinib kwa ajili ya kutibu wagonjwa mahututi  wa COVID-19.Dawa nyingine iliyopendekezwa na wataalamu hao ni Monoclonal, na pia kutoa masharti ya matumizi ya kingamwili hiyo kutumika kwa wagonjwa walio na Covid-19 isiyo kali, lakini tu kwa wale walio katika hatari kubwa ya kulazwa hospitalini.

Wanawake wanasimama katika mstari wa kupokea chanjo yao ya COVID-19 katika Kijiji cha Chiwinga katika Wilaya ya Kasungu, Kati ya Malawi Jumanne, Desemba 14, 2021. UNICEF/2021/THOKOCHIKONDI.
© UNICEF/ Thoko Chikondi

Omicron ilichochea wimbi la Covid-19 barani Afrika lakini inapungua haraka 

Baada ya wimbi la ugonjwa wa Covid-19 lililodumu kwa takribani wiki sita, wimbi hilo la nne barani Afrika ambalo kimsingi lilichochewa na mnyumbuliko wa virusi vya corona kwa jina Omicron, sasa linapungua na hivyo kulifanya kuwa wimbi lililodumu kwa muda mfupi zaidi katika bara hilo ambako jumla ya maambukizi hivi sasa tangu kuibuka kwa ugonjwa huo limezidi milioni 10. Imeeleza taarifa ya shirika la afya la Umoja wa Mataifa kanda ya Afrika iliyotolewa hii leo Brazzaville nchini Congo.  

Sauti
2'23"

13 JANUARI 2022

Miongoni mwa tuliyonayo hii leo katika habari za Umoja wa Mataifa


Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa, WHO linasema kuwa japokuwa habari mbayá ni kuwa Omicron ambao ni mnyumbuliko wa virusi vya corona ulichochea wimbi la nne la Covid-19 barani Afrika lakini unapungua haraka kuliko mawimbi yaliyotangulia kama lile la mnyumbuliko aina ya Delta. Hata hivyo idadi ya waliopata chanjo dhidi ya Covid-19 barani humo baado ni ndogo mno.  

Sauti
12'31"
Mfanyakazi wa afya aliyevaa vifaa kamili vya kujikinga (PPE) anamfanyia mgonjwa wa kike kipimo cha COVID-19 katika kliniki.
©UNDP/Abed Zagout

Omicron isidharauliwe na kukosa usawa wa chanjo kunatuumiza zaidi - WHO

“Kutokana na kuenea kwa mnyumbuliko mpya wa omicron katika maeneo yote duniani, maambukizi mapya yalifikia milioni 9.5 na vifo vilizidi 41,000 ulimwenguni kuanzia Desemba 27 hadi Januari 2. "Na tunajua kwamba namba hizi ziko chini ya zile halisi." Anaonya Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Afya la Umoja wa Mataifa, Dkt Tedros Ghebreyesus akitoa wito kwa mara nyingine tena kwa usambazaji sawa wa chanjo dhidi ya virusi vya corona. 

Uwanja mtupu wa soka wenye koni za goli na mazoezi, na mandhari ya jiji nyuma.
UN News/Anton Uspensky

Kampeni ya #ACTogether kutumika wakati wa Kombe la Kiarabu la FIFA

Kwa kutumia jukwaa la Kombe la kwanza la Kiarabu la FIFA™, Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa, WHO, FIFA na mamlaka ya Qatar wanazindua kampeni ya #ACTogether ili kutoa wito wa ushirikiano na umoja ili kuhakikisha upatikanaji sawa wa chanjo, matibabu na vipimo vya ugonjwa unaosababishwa na virusi vya corona, COVID-19.

WHO-Europe

WHO yatoa muongozo wa vyeti vya chanjo ya COVID-19 kielektronik

Shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, WHO linasema ingawa haliungi mkono mahitaji ya uthibitisho wa chanjo ya COVID-19 ili mtu kuweza kusafiri lakini katika mazingira mengine kulingana na tathmini ya hatari ya nchi zinazohusika, taarifa kuhusu chanjo dhidi ya COVID-19 zinaweza kutumika kupunguza mahitaji ya karantini au upimaji wakati wa kuwasili katika nchi hizo. 

(Taarifa ya Anold Kayanda) 

Sauti
1'43"
Mwanamke aliyevaa hijabu nyeusi ameshika cheti cha chanjo ya kijani kibichi.
Mohamed Yassin

Kuelekea kuhifadhi taarifa za chanjo ya Covid-19 kidijitali, WHO yatoa mwongozo

Shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, WHO linasema ingawa haliungi mkono mahitaji ya uthibitisho wa chanjo ya COVID-19 ili mtu kuweza kusafiri lakini katika mazingira mengine kulingana na tathmini ya hatari ya nchi zinazohusika, taarifa kuhusu chanjo dhidi ya COVID-19 zinaweza kutumika kupunguza mahitaji ya karantini au upimaji wakati wa kuwasili katika nchi hizo.

Sauti
1'43"