Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
Virusi vya corona vilibadilisha matarajio yangu katika UN lakini nimejifunza SDGs-Loise Wairimu
Janga la ugonjwa wa COVID-19 unaosababishwa na virusi vya Corona limevuruga ndoto za mamilioni ya watu kote duniani. Elimu, afya, biashara, utalii, ukuaji wa kiuchumi na kadhalika vimeyumba kwa kiasi kikubwa.
Kampeni ya kutulia kwanza yaani #PledgetoPause yazinduliwa
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akizindiua hatua ya kuzuia usambazaji wa taarifa za uongo mitandaoni, ametoa wito kwa watu kote ulimwenguni kutoa ahadi ya kutulia kwanza kabla ya kusambaza taarifa mitandaoni.
Tunawasihi watu wote duniani kuahidi kutulia kwanza kabla ya kusambaza taarifa mtandaoni-UN
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akizindiua hatua ya kuzuia usambazaji wa taarifa za uongo mitandaoni, ametoa wito kwa watu kote ulimwenguni kutoa ahadi ya kutulia kwanza kabla ya kusambaza taarifa mitandaoni.
Utafiti waonesha mtoto 1 kati ya 6 anaishi katika umaskini uliokithiri.
Tathimini ya utafiti uliofanywa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF na Benki ya Dunia iliyotolewa hii leo mjini New York na Washington DC Marekani imekadiria kuwa mtoto 1 kati ya 6 au sawa na watoto milioni 356 duniani kote, walikuwa wanaishi katika umaskini uliokithiri hata kabla ya janga la virusi vya corona, na hali inategemewa kuwa mbaya zaidi. Ahimidiwe Olotu na maelezo zaidi.
Mtoto 1 kati ya 6 anaishi katika umaskini uliokithiri-Utafiti
Tathimini ya utafiti uliofanywa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF na Benki ya Dunia iliyotolewa hii leo mjini New York na Washington DC Marekani imekadiria kuwa mtoto 1 kati ya 6 au sawa na watoto milioni 356 duniani kote, walikuwa wanaishi katika umaskini uliokithiri hata kabla ya janga la virusi vya corona, na hali inategemewa kuwa mbaya zaidi.
UNICEF yajiandaa kwa ajili ya chanjo dhidi ya COVID-19
Wakati duniani inasubiri kwa hamu chanjo dhidi ya ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICF, nalo limeanza maandalizi ya kuhakikisha chanjo hiyo inatolewa na kusambazwa mapema na kwa usalama kwa kununua na kuhifadhi mabomba ya sindano na vifaa vingine vya kufanikisha zoezi hilo.
UNICEF kuandaa sindano na mabomba ya utoaji chanjo dhidi ya COVID-19
Wakati duniani inasubiri kwa hamu chanjo dhidi ya ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICF, nalo limeanza maandalizi ya kuhakikisha chanjo hiyo inatolewa na kusambazwa mapema na kwa usalama kwa kununua na kuhifadhi mabomba ya sindano na vifaa vingine vya kufanikisha zoezi hilo.
Uhaba wa watu kunawa mikono kwa sabuni unawaweka mamilioni kwenye hatari kubwa zaidi
Ingawa kunawa mikono kwa sabuni ni muhimu katika mapambano dhidi ya magonjwa ya kuambukiza ikiwemo COVID-19, mamilioni ya watu duniani hawana mahali pa kunawia mikono, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF katika siku ya kimataifa ya kunawa mikono hii leo.
Wakimbizi wa Kisomali waungana kusaidia wenyeji wao, wahamiaji na wasaka hifadhi Afrika Kusini.
Nchini Afrika Kusini, jamii ya wakimbizi wa Kisomali wameamua kushirikiana na majirani zao raia wa Afrika Kusini kuwasaidia watu ambao wanahangaika na maisha katika kipindi hiki cha janga la COVID-19 nchini humo.
13 OKTOBA 2020
Katika jarida la habari la Umoja wa Mataifa hii leo, Flora Nducha anakuletea
-Katika siku ya kimataifa ya kupunguzahatari za majanga Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa antonio Guterres ameonya kwamba bila udhibiti mzuri wa hatari za majanga , hali ambayo ni mbaya itazidi kubwa mbaya zaidi
-Mashirika ya Umoja wa Mataifa ya FAO, IFAD, WHO na ILO leo katika taarifa yao ya pamoja yameonya kwamba COVID-19 mbali ya kuathiri afya inaathiri maisha ya watu na mifumo ya chakula hivyo hatua zichukuliwe haraka kunusuru janga zaidi