Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

Uwanja wa michezo New York
UN News/ Anton Uspensky

Kampeni ya #ACTogether kutumika wakati wa Kombe la Kiarabu la FIFA

Kwa kutumia jukwaa la Kombe la kwanza la Kiarabu la FIFA™, Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa, WHO, FIFA na mamlaka ya Qatar wanazindua kampeni ya #ACTogether ili kutoa wito wa ushirikiano na umoja ili kuhakikisha upatikanaji sawa wa chanjo, matibabu na vipimo vya ugonjwa unaosababishwa na virusi vya corona, COVID-19.