Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

Shughuli za ununuzi kwenye duka jijini Dar es Salaam, Tanzania wakati ugonjwa wa Corona ulivyoripotiwa Tanzania mwezi Machi mwaka huu.
UN News/ Stella Vuzo

Tanzania yashauriwa kujiunga na mpango wa chanjo wa COVAX 

Kamati iliyoundwa na Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kufanya tathmini juu ya Ugonjwa wa COVID-19 imependekeza taifa hilo kukubali Chanjo na kujiunga na COVAX ambao ni mkakati wa kimataifa wa kuhakikisha kila nchi inapata chanjo unaosimamiwa na shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO.