Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

University of Oxford/John Cairns

Njia pekee ya kupambana na janga hili ni kuhakikisha chanjo inapatikana kwa gharama nafuu kwa kila mtu dunian-UN

Wataalam wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa leo wamezikosoa nchi zinazojaribu kubinafsisha na kuhodhi chanjo yoyote ya dhidi ya corona au COVID-19 inayotarajiwa kupatikana wakisema njia pekee ya kupambana na janga hili ni kuhakikisha chanjo inapatikana kwa gharama nafuu kwa kila mtu duniani.

Sauti
2'22"
Hifadhi zinachukua hatua kukabiliana na COVID-19 na kuhakikisha utalii salama.Simba katika hifadhi ya Masai Mara nchini Kenya
UNEP GRID Arendal/Peter Prokosch

Hifadhi ya Dja Cameroon yachukua hatua kupambana na COVID-19 

Maeneo mengi ya hifadhi za viumbe hai na misitu pamoja na mbuga za wanyama pori yameathirika kwa namna moja au nyingine kutokana na uwepo wa mlipuko vya virusi vya corona ulimwenguni. Hifadhi ya Dja nchini Cameroon ni miongoni mwa waathirika, lakini ambao wanafanya chini juu kujikinga na kujikwamua na hali hiyo.

Sauti
1'49"
Kijana Tanzania atengeneza ndoo ya kunawa mikono bila kugusa koki wala sabuni.
UN News/ UNIC Tanzania

COVID-19 inahimiza ubunifu wa kiafya barani Afrika-WHO

Utafiti mpya wa Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa WHO uliotangazwa katika mji mkuu wa Jamhuri ya Congo, Brazzaville, umesema janga la COVID-19 limeongeza nguvu kwenye maendeleo ya ubunifu zaidi ya 120 wa teknolojia ya afya ambao umejaribiwa au kupitishwa barani Afrika.

Sauti
2'51"
© UNHCR/Rocco Nuri

Mashahiri yatumika kupinga ukatili kwa watoto miongoni mwa wakimbizi Uganda wakati wa COVID-19  

Kufuatia mlipuko wa COVID-19 mnamo Machi mwaka huu nchini Uganda, shule zilifungwa na hivyo kuwaweka hatarini watoto kukumbana na ukatili wa kijinsia hasa katika makazi ya wakimbizi ambako huduma nyingi huwa hazitoshelezi jamii hizo. Kwa mantiki hiyo, shirika la Umoja wa Mataifa kupitia wadau wake wamekuwa wakitumia mbinu mbalimbali kuhamasisha jamii kuhakikisha ulinzi wa watoto wa kike na wale wa kiume. Sasa, watoto wenyewe wanashirikishwa katika kampeni ya kuwalinda kwa kuwapatia nafasi ya kuzungumzia changamoto na mikakati ya kuzikabili. 

Sauti
3'29"