Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
04 JANUARI 2021
Katika Jarida la Habari za umoja wa Mataifa hii leo Flora Nducha anakuletea
-Watu zaidi ya 100 wauawa katika shambulio kwenye jimbo la Tillaberi nchini Niger, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa alaani vikali shambulio hilo na kutaka wahusika wakamatwe na kuwajibishwa.
-Nchini Pakistan wachimba migodi ya makaa ya mawe 11 wameuawa katika shambulio la kigaidi lililotokea mwishoni mwa wiki kwenye jimbo la Balouchistan, watu wengine wengi wamejerihiwa na wengine kutekwa .
UNICEF yagawa redio za sola 10,000 kusaidia watoto kusoma wakijiandaa kurejea shule Kenya
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF , nchini Kenya, limegawa redio 10,000 zinazotumia nishati ya sola kwa kaya masikini nchini humo ili watoto wengi wapate fursa ya kusoma nyumbani wakati huu wakijianda kurejea shuleni.
Tuna njaa, ni maafa, asema mkimbizi wa Syria aliyeko Lebanon. UNHCR inajitahidi kusaidia.
Ripoti hiyo ya Benki ya Dunia na UNHCR imechunguza madhara ya ugonjwa wa COVID-19 katika kuwasukuma wakimbizi wa Syria katika umaskini, wao pamoja na wenyeji wao nchini Jordan, Lebaon na aneo la Kurd nchini Iraq. Ahimidiwe Olotu na taarifa zaidi.
Ripoti hiyo inasema watu wanaokadiriwa kufikia milioni 4.4 katika jamii wenyeji, na pia takribani wakimbizi milioni moja wa Syria, na Wairaq wengine 180,000 waliokimbia makazi yao wameanguka chini ya mstari wa umaskini tangu mwanzo wa janga la COVID-19.
Ni maafa mazito, tuna njaa, asema mkimbizi wa Syria aliyeko Lebanon. UNHCR inajitahidi kusaidia.
Ripoti hiyo ya Benki ya Dunia na UNHCR imechunguza madhara ya ugonjwa wa COVID-19 katika kuwasukuma wakimbizi wa Syria katika umaskini, wao pamoja na wenyeji wao nchini Jordan, Lebaon na aneo la Kurd nchini Iraq.
COVID-19 inaongezeka Afrika, hatua thabiti zinahitajika-WHO
Maambuki ya COVID-19 katika ukanda wa Afrika yameongezeka kwa kasi katika miezi miwili iliyopita, hali hiyo ikisisitiza hitaji la hatua za afya za umma zilizoimarishwa ili kuzuia kuongezeka kwa maambukizi, hasa wakati watu wanapokusanyika au kusafiri kwa sherehe za mwisho wa mwaka, imeeleza taarifa ya shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO, iliyotolewa hii leo mjini Brazzaville, Jamhuri ya Congo.
WHO yazindua kampeni ya mwaka mzima kusaidia watu milioni 100 kuacha tumbaku
WHO leo imezindua kampeni ya mwaka mzima kwa jina "Jitolee kuacha kuvuta." kwa ajili ya maadhimisho ya siku ya kimataifa ya kutovuta tumbaku kwa mwaka ujao wa 2021.
UNICEF yahimiza serikali duniani kufungua shule, japo kwa tahadhari
Idadi ya watoto wa shule walioathiriwa na kufungwa kwa shule kutokana na janga la ugonjwa wa Corona au COVID-19 imeongezeka kwa asilimia 38 mwezi uliopita wa Novemba, hali hiyo ikiweka mkwamo mkubwa kwenye maendeleo ya masomo na ustawi wa wanafunzi zaidi ya milioni 90 ulimwenguni, limeeleza shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF.
Dola milioni 818 zinahitajika kutoa huduma muhimu na za kuokoa maisha kwa wanawake na wasichana walioathiriwa na mizozo-UNFPA
Shirika la idadi ya watu la Umoja wa Mataifa, UNFPA, leo limezindua ombi lake kubwa kuliko yote la msaada wa kibinadamu.
Maskini wataongezeka kufikia zaidi ya watu bilioni moja. Nchi maskini kuathirika zaidi-UN
Ripoti mbili kutoka mashirika ya Umoja wa Mataifa zilizotolewa hii leo, kwa namna tofauti zimeonesha namna athari za ugonjwa wa COVID-19 unaosababishwa na virusi vya corona, zikavyosababisha kuporomoka kwa nguvu ya uchumi ya watu wengi na hivyo kuwaingiza katika umaskini uliokithiri.
Ujumbe wangu kwa G20 ni rahisi: Tunahitaji mshikamano na ushirikiano-Guterres
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akiwahutubia wanahabari hii leo mjini New York Marekani, kuhusu mkutano wa kesho wa viongozi wa nchi 20 zilizo na uchumi mkubwa duniani, G20, ameanza kwa kueleza kuwa mkutano huu unakuja wakati ambao janga la COVID-19 linaendelea kuuharibu ulimwengu.