Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

Picha ya makataba ikiwaonesha wanahabari wakipiga picha za video katika Makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani.
UN Photo/Ariana Lindquist

Wanahabari wanapolengwa, jamii kwa ujumla ndiyo inalipia gharama-Guterres

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kupitia Ujumbe wake alioutoa hii leo mjini New York Marekani kuhusu siku  ya leo ya kimataifa ya kutokomeza ukwepaji wa sheria ya uhalifu dhidi ya wanahabari, amesema katika siku ya mwaka huu, dunia vikiwemo vyombo vya habari, juu ya changamoto nyingine, vimekabiliwa na changamoto mpya kabisa ambayo ni COVID-19. 

Sauti
2'50"

30 Oktoba 2020

Katika kuelekea siku ya miji duniani hapo kesho Oktoba 31, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Abtonio Guterres kupitia ujumbe maalum wa siku hiyo amesema miji imebeba gharama kubwa ya janga la corona au COVID-19 lakini jamii katika miji hiyo zimedhihirisha thamani yake katika kukabiliana nalo.

Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula WFP kwa kushirikiana na serikali ya Kenya leo wamezindua mpango wa ugawaji fedha taslim kwa familia 24,000 mjini Mombasa  katika makazi yasiyo rasmi ambao Maisha yao yamesambaratishwa na athari za janga la COVID-19.

Sauti
10'48"
Wanafunzi waliporejea darasani katika shule ya msingi San Pedro Kusini Magharibi mwa Côte d'Ivoire.
© UNICEF/Frank Dejo

Watoto katika nchi maskini wamepoteza miezi minne ya masomo tangu kuanza kwa janga la COVID-19-Ripoti 

Watoto wa shule katika nchi zenye kipato cha chini na cha kati chini, tayari wamepoteza takribani miezi minne ya masomo tangu kuanza kwa janga la virusi vya corona ikilinganishwa na wiki sita za upotezaji masomo katika nchi zenye kipato cha juu. Hiyo ni kwa mujibu wa ripoti iliyochapishwa hii leo mjini New York na Washington Marekani pamoja na Paris Ufaransa na mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la elimu, sayansi na utamaduni UNESCO na la kuhudumia watoto UNICEF kwa kushirikiana na  Benki ya Dunia. 

Sauti
2'57"
Uwekezaji mkubwa kama huu wa bwawa katika Mto Nura nchini Kazakhstan mara nyingi unahitaji uwekezaji wa moja kwa moja wa nje.
World Bank/Shynar Jetpissova

COVID-19 imeangusha kwa asilimia 49 aina zote za uwekezaji wa nje wa nchi zilizoendelea.

Mtiririko wa uwekezaji wa moja kwa moja wa kigeni kimataifa, FDI, umepungua kwa asilimia 49 katika nusu ya kwanza ya 2020 ikilinganishwa na mwaka 2019, kwa sababu ya kuanguka kwa uchumi kutokana na COVID-19, umebaini utafiti wa hivi karibuni wa  Monitor mwelekeo wa uwekezaji uliofanywa na shirika la Umoja wa Mataifa la biashara na maendeleo UNCTAD na kutolewa leo tarehe 27 Oktoba 2020.