Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
WHO yatoa vifaa na mafunzo kupambana na COVID-19 Beirut
Shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO linatoa msaada wa aina mbalimbali kusaidia vita dhidi ya janga la corona au COVID-19 nchini Lebanon hasa kutokana na kuongezeka kwa idadi ya wagonjwa baada ya milipuko iliyotokea mwezi Agosti mwaka huu mjini Beirut.
Janga la COVID-19 halijamalizika , muwe makini katika matumizi yenu:IMF
Shirika la fedha duniani IMF limeziasa nchi na watu wote kuwa makini katika matumizi yao kwani athari za kiuchumi zilizosababishwa na janga la corona au COVID-19 hazijaisha na zitaendelea kwa muda.
Mipango kabambe ya kufanikisha watoto kwenda shuleni Kenya
Nchini Kenya, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF kwa kushirikiana na serikali ya Japan, limechukua hatua kuhakikisha wanafunzi wanaorejea shuleni, wanakuwa salama dhidi ya ugonjwa virusi unaosababishwa na virusi vya Corona au COVID-19.
Wanahabari wanapolengwa, jamii kwa ujumla ndiyo inalipia gharama-Guterres
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kupitia Ujumbe wake alioutoa hii leo mjini New York Marekani kuhusu siku ya leo ya kimataifa ya kutokomeza ukwepaji wa sheria ya uhalifu dhidi ya wanahabari, amesema katika siku ya mwaka huu, dunia vikiwemo vyombo vya habari, juu ya changamoto nyingine, vimekabiliwa na changamoto mpya kabisa ambayo ni COVID-19.
30 Oktoba 2020
Katika kuelekea siku ya miji duniani hapo kesho Oktoba 31, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Abtonio Guterres kupitia ujumbe maalum wa siku hiyo amesema miji imebeba gharama kubwa ya janga la corona au COVID-19 lakini jamii katika miji hiyo zimedhihirisha thamani yake katika kukabiliana nalo.
Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula WFP kwa kushirikiana na serikali ya Kenya leo wamezindua mpango wa ugawaji fedha taslim kwa familia 24,000 mjini Mombasa katika makazi yasiyo rasmi ambao Maisha yao yamesambaratishwa na athari za janga la COVID-19.
WFP na serikali ya Kenya wazindua mpango usaidizi wa kifedha kwa familia zilizoathiriwa na COVID-19 Mombasa, Kenya
Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula WFP kwa kushirikiana na serikali ya Kenya leo wamezindua mpango wa ugawaji fedha taslim kwa familia 24,000 mjini Mombasa, Kenya katika makazi yasiyo rasmi ambao maisha yao yamesambaratishwa na athari za janga la COVID-19.
Watoto katika nchi maskini wamepoteza miezi minne ya masomo tangu kuanza kwa janga la COVID-19-Ripoti
Watoto wa shule katika nchi zenye kipato cha chini na cha kati chini, tayari wamepoteza takribani miezi minne ya masomo tangu kuanza kwa janga la virusi vya corona ikilinganishwa na wiki sita za upotezaji masomo katika nchi zenye kipato cha juu. Hiyo ni kwa mujibu wa ripoti iliyochapishwa hii leo mjini New York na Washington Marekani pamoja na Paris Ufaransa na mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la elimu, sayansi na utamaduni UNESCO na la kuhudumia watoto UNICEF kwa kushirikiana na Benki ya Dunia.
COVID-19 imetufunza mengi na hata ambayo hatukutarajia: Barubaru Termeh na Toranj
Kutana na mapacha wawili barubaru kutoka nchini Iran, wanasema janga la corona au COVID-19 limewafunza mengi, kuanzia kusomea nyumbani, kukabiliana na upweke na msongo wa mawazo na hata kupika na majukumu mengine ya nyumbani.
COVID-19 imeangusha kwa asilimia 49 aina zote za uwekezaji wa nje wa nchi zilizoendelea.
Mtiririko wa uwekezaji wa moja kwa moja wa kigeni kimataifa, FDI, umepungua kwa asilimia 49 katika nusu ya kwanza ya 2020 ikilinganishwa na mwaka 2019, kwa sababu ya kuanguka kwa uchumi kutokana na COVID-19, umebaini utafiti wa hivi karibuni wa Monitor mwelekeo wa uwekezaji uliofanywa na shirika la Umoja wa Mataifa la biashara na maendeleo UNCTAD na kutolewa leo tarehe 27 Oktoba 2020.
Loise Wairimu-Virusi vya corona vilibadilisha matarajio yangu katika UN lakini nimejifunza SDGs
Janga la ugonjwa wa COVID-19 unaosababishwa na virusi vya Corona limevuruga ndoto za mamilioni ya watu kote duniani. Elimu, afya, biashara, utalii, ukuaji wa kiuchumi na kadhalika vimeyumba kwa kiasi kikubwa. Assumpta Massoi na maelezo zaidi.