Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
Makazi kwa wote ndio chachu ya mustakbali bora mijini:UN-HABITAT
Kuwa makazi bora hivi sasa kuliko wakati mwingine wowote ni suala la uhai na kifo hasa janga la corona likiendelea kusambaa duniani na watu wakitakiwa kusalia majumbani, lakini hatua hiyo haiwezekani hasa kwa wale ambao hawana wanapopaita nyumbani limesema shirika la Umoja wa Mataifa la makazi UN-HABITAT.
Kutoka darasani hadi shambani, mwalimu kutoka Uganda azungumza
Leo ikiwa ni siku ya walimu duniani, ambayo mwaka huu inaadhimishwa kukiwa na changamoto kubwa kwa walimu na wanafunzi kufuatia janga la corona au COVID-19, huku Umoja wa Mataifa ukisema takriban wanafunzi bilioni 1.6 ambao ni zaidi ya wanafunzi wote duniani waliojiandikisha shule wameathiriwa na kufungwa kwa shule.
05 Oktoba 2020
COVID-19 yamlazimisha mwalimu kusaka kipato mbadala nchini Uganda. UN-HABITAT yachukua hatua kupambana na COVID-19 hata kwa wasio na makazi Kenya. Elimu ya IFAD yawasaidia wanawake wa Kontagora, Nigeria kuwa mamilionea.
COVID-19 yamlazimisha mwalimu kusaka kipato mbadala nchini Uganda
Leo ikiwa ni siku ya walimu duniani, ambayo mwaka huu inaadhimishwa kukiwa na changamoto kubwa kwa walimu na wanafunzi kufuatia janga la corona au COVID-19, huku Umoja wa Mataifa ukisema takriban wanafunzi bilioni 1.6 ambao ni zaidi ya wanafunzi wote duniani waliojiandikisha shule wameathiriwa na kufungwa kwa shule.
UN-HABITAT yachukua hatua kupambana na COVID-19 hata kwa wasio na makazi Kenya
Ikiwa leo ni siku ya makazi duniani, kuwa na makazi bora imeelezwa hivi sasa kuliko wakati mwingine wowote ni suala la uhai na kifo hasa janga la corona au COVID-19 likiendelea kusambaa duniani na watu wakitakiwa kusalia majumbani, lakini hatua hiyo haiwezekani hasa kwa wale ambao hawana wanapopaita nyumbani limesema shirika la Umoja wa Mataifa la makazi UN-HABITAT.
1 Oktoba 2020
Hii leo mkutano wa 75 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA75 unakuwa na kikao cha ngazi ya juu kuhusu kuchagiza utekelezaji wa usawa wa jinsia na uwezeshaji wanawake na mtoto wa kike, sambamba na maadhimisho ya miaka 25 tangu mkutano wa 4 wa kimataifa kuhusu wanawake uliofanyika Beijing nchini China mwaka 1995.
Changamoto kwangu ni fursa ya kujifunza asema Fiona Beine mlinda amani raia wa Uganda nchini Iraq.
Wazee lazima wawe kipaumbele katika juhudi zetu za kuishinda COVID-19-Guterres
Watu wenye ulemavu, COVID-19 imetuathiri maradufu-UGANDA
Mwandishi wetu wa Uganda, John Kibego ameangazia changamoto zinazowakabili watu wenye ulemavu hasa wanawake kutokana na vizuizi vilivyosababishwa na mlipuko wa COVID-19 nchini Uganda.
Wazee lazima wawe kipaumbele katika juhudi zetu za kuishinda COVID-19-Guterres
Ulimwengu unaadhimisha miaka 30 ya Siku ya Wazee duniani tunapotathimi athari mbaya na kali ambazo janga la COVID-19 limesababisha kwa wazee ulimwenguni kote, sio tu kwa afya zao, bali pia juu ya haki zao na ustawi wao, amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kupitia ujumbe wake alioutoa hii leo kuhusu Siku ya leo ya Kimataifa ya wazee duniani na kisha akashauri.
COVID-19 imetupa mafunzo-Uganda
Tunauona ushirikiano wa kimataifa kama njia ya kushughulikia matishio magumu na mapya kama vile janga la COVID-19 ambalo limeathiri kila mwanachama wa jumuiya ya kimataifa, imeeleza sehemu ya kwanza ya hotuba ya Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda katika mjadala mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ambayo imesomwa kwa niaba yake na Naibu Mwakilishi wa kudumu wa Uganda katika Umoja wa Mataifa, Balozi Philip Ochen Odida ikieleza pamoja na mengine, kile ambacho wamejifunza kutokana na ugonjwa huo.
Manusura wa COVID-19 waandika barua kudai chanjo yenye utu, isiyojali kipato cha mtu
Manusura wa ugonjwa wa Corona au COVID-19 kutoka mataifa 37 duniani ni miongoni mwa watu waliopaza sauti kutaka chanjo dhidi ya ugonjwa huo itakapopatikana iweze kumfikia kila mtu popote pale alipo bila kujali hali yake ya kiuchumi au kijamii na isiwe na hataza.