Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

05 Oktoba 2020

COVID-19 yamlazimisha mwalimu kusaka kipato mbadala nchini Uganda. UN-HABITAT yachukua hatua kupambana na COVID-19 hata kwa wasio na makazi Kenya. Elimu ya IFAD yawasaidia wanawake wa Kontagora, Nigeria kuwa mamilionea.  

Sauti
13'19"
Mradi wa UN-HABITAT nchini Kenya unaosaidia wasio na makazi katika kukabiliana na ugonjwa wa virusi vya corona.
UN News/ Jason Nyakundi

UN-HABITAT yachukua hatua kupambana na COVID-19 hata kwa wasio na makazi Kenya

Ikiwa leo ni siku ya makazi duniani, kuwa na makazi bora imeelezwa hivi sasa kuliko wakati mwingine wowote ni suala la uhai na kifo hasa janga la corona  au COVID-19 likiendelea kusambaa duniani na watu wakitakiwa kusalia majumbani, lakini hatua hiyo haiwezekani hasa kwa wale ambao hawana wanapopaita nyumbani limesema shirika la Umoja wa Mataifa la makazi UN-HABITAT.

Sauti
2'37"

1 Oktoba 2020

Hii leo mkutano wa 75 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA75 unakuwa na kikao cha ngazi ya juu kuhusu kuchagiza utekelezaji wa usawa wa jinsia na uwezeshaji wanawake na mtoto wa kike, sambamba na maadhimisho ya miaka 25 tangu mkutano wa 4 wa kimataifa kuhusu wanawake uliofanyika Beijing nchini China mwaka 1995. 

Changamoto kwangu ni fursa ya kujifunza asema Fiona Beine mlinda amani raia wa Uganda nchini Iraq.

Wazee lazima wawe kipaumbele katika juhudi zetu za kuishinda COVID-19-Guterres  

Sauti
13'32"
Wanawake wazee katika moja ya kambi ya wazee inayohudumiwa na serikali nchini Msumbiji.
World Bank/ Eric Miller

Wazee lazima wawe kipaumbele katika juhudi zetu za kuishinda COVID-19-Guterres  

Ulimwengu unaadhimisha miaka 30 ya Siku ya Wazee duniani tunapotathimi athari mbaya na kali ambazo janga la COVID-19 limesababisha kwa wazee ulimwenguni kote, sio tu kwa afya zao, bali pia juu ya haki zao na ustawi wao, amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kupitia ujumbe wake alioutoa hii leo kuhusu Siku ya leo ya Kimataifa ya wazee duniani na kisha akashauri.  

Sauti
2'2"
Balozi Philip Ochen Odida, Naibu Mwakilishi wa kudumu wa Uganda katika Umoja wa Mataifa akihutubia mjadala mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA75
UN Photo/Loey Felipe

COVID-19 imetupa mafunzo-Uganda 

Tunauona ushirikiano wa kimataifa kama njia ya kushughulikia matishio magumu na mapya kama vile janga la COVID-19 ambalo limeathiri kila mwanachama wa jumuiya ya kimataifa, imeeleza sehemu ya kwanza ya hotuba ya Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda katika mjadala mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ambayo imesomwa kwa niaba yake na Naibu Mwakilishi wa kudumu wa Uganda katika Umoja wa Mataifa, Balozi Philip Ochen Odida ikieleza pamoja na mengine, kile ambacho wamejifunza kutokana na ugonjwa huo.