Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Tusiwasahau wakimbizi wa Congo na shida wanazopitia UNHCR/ CHRISTINA

Tusiwasahau wakimbizi wa Congo na shida wanazopitia UNHCR/ CHRISTINA

Pakua

Msanii mashuhuri wa Ufaransa  Christine pamoja na kundi lake the Queens wametoa wito kwa mashirika  ya kibinadamu na wahisani kutopuuzia  suala  la machafuko yanayoendelea Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo DRC  na kusababisha wimbi kubwa la wakimbizi wanaofungasha virago kila uchao.

Akitoa wito huo wakati alipotembelea kambi ya wakimbizi wa kutoka DRC walioko Kusini Magharibi mwa Uganda , Christina amesema anajaribu kutumia nafasi yake kama msanii wa muziki na pia mtu mashuhuri kupaza sauti kwa jamii ya kimataifa  na wahisani kutosahau  zahma wanazopitia wakimbizi.

Katika ziara yake hiyo Christina alipatafursa ya kutemebelea pia kituo cha mafunzo kwa vijana wakimbizi  cha Rwamwanja kilichopo chini ya usimamizi wa  shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR na kusema amefurahiswa na jitiahda za UNHCR kuwapa vijana fursa ya kijifunza muziki na pia michezo mbalimbali wakiti wakiwa katika hali ngumu kambini.

Bwana Bornwell kantande ambaye ni mwakilishi wa UNHCR nchini Uganda amesema nchini hiyo inahifadhi zaidi ya wakimbizi milioni 1.4  kutoka ukanda wa Afrika Mashariki kama Burundi,Sudan kusini, na zaidi ya laki 230 wanatoka DRC.

Photo Credit
Wakimbizi nchini DRC. Picha: © UNHCR/M.Brook