Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

UNICEF

Watoto wakijifunza kwa kutumia kompyuta ndogo au tablet katika Shule ya Umma ya Melen ya Yaoundé, Kamerun.
© UNICEF/Frank Dejongh

Ukweli kuhusu dhana nne potofu kuhusu usalama wa mtoto mtandaoni

Maisha ya watoto na vijana kwa muda mrefu yameunganishwa na intaneti na mitandao ya kijamii na kadri teknolojia inavyoendelea kubadilika kwa kasi jambo hili linaongezeka na kuenea zaidi na kuruhusu watoto kufikia ulimwengu wa habari, kujifunza, kushirikiana, burudani na zaidi inaweza kuwa chanya lakini wakati mwingine kuna hatari, linaeleza shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto UNICEF katika makala hii iliyochapishwa kwenye wavuti wa shirika hilo leo Siku ya Kimataifa ya intaneti salama.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres (Picha ya maktaba)
United Nations/Cyril Bailleul

HABARI KWA UFUPI: Katibu Mkuu UN ahutubia BRICS. Pia kuna Myanmar vilevile UNICEF na hatima ya watoto Sudan

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amehutubia mkutano wa viongozi kundi la Brazil, Urusi, India, China na Afrika Kusini au BRICS huko Johannesburg Afrika Kusini na kusema katika dunia ya sasa iliyogawanyika na kugubikwa na majanga hakuna mbadala mwingine wa kuwezesha kusonga mbele zaidi ya mshikamano hasa kwenye masuala lukuki ikiwemo marekebisho ya mfumo wa kimataifa wa fedha duniani.  

 

Ili kupata watoto wake, Nirere alienda katika ofisi ya CAJED iliyoko Kanyaruchinya, DRC ambapo picha za watoto waliotenganishwa na familia zao zinaoneshwa.
©UNICEF/Benekire

Zaidi ya matukio 300,000 ya ukatili dhidi ya watoto walio katika migogoro yathibitishwa duniani kote

Matukio 315,000 ya ukiukwaji haki dhidi ya watoto walio katika migogoro yamethibitishwa na Umoja wa Mataifa kati ya mwaka 2005 na mwaka 2022, hicho kikiwa ni kielelezo tosha cha athari mbaya za vita na migogoro kwa Watoto, imeeleza taarifa ya shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, UNICEF iliyotolewa leo jijini New York, Marekani na katika mji mkuu wa Norway, Oslo ambako leo na kesho unafanyika mkutano kuhusu Kulinda Watoto katika Migogoro yenye kutumia Silaha. 

Sauti
2'18"
Mama amempeleka mwanye aliyeathirika vibaya na utapiamlo kwenye kituo cha lishe cha WFP Torit nchini Sudan Kusini
© WFP/Eulalia Berlanga

Mabadiliko ya tabianchi yazidisha zahma ya utapiamlo na njaa Sudan Kusini:UNICEF/FAO/WFP 

Umoja wa Mataifa umeonya hii leo kuwa njaa na utapiamlo vinaongezeka katika maeneo yote yaliyokumbwa na mafuriko, ukame na mizozo nchini Sudan Kusini huku baadhi ya jamii zikiwa hatarini kukumbwa na njaa iwapo misaada ya kibinadamu haitakuwa endelevu, halikadhalika mikakati ya kukabili madhara ya mabadiliko ya tabianchi haitaimarishwa.