Hali ya kibinadamu Syria bado ni mateso matupu- Mueller
Msaidizi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu masuala ya kibinadamu na msaada wa dharura, Ursula Mueller, amesema hali bado ni tete nchini Syria kufuatia mapigano ya wenyewe kwa wenyewe yaliyodumu kwa zaidi ya miaka saba sasa.
Katika taarifa yake kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa hii leo kuhusu Syria, Bi. Mueller amesema mgogoro huo umesababisha mateso makubwa kwa wananchi, vifo vingi kwa raia na huku wengine wakijeruhiwa au kutojulikana waliko.