Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

UN affairs, SG

Hali ya kibinadamu Syria bado ni mateso matupu- Mueller

Msaidizi wa Katibu  Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu masuala ya kibinadamu na msaada wa dharura, Ursula Mueller, amesema hali bado ni tete nchini Syria kufuatia mapigano ya wenyewe kwa wenyewe yaliyodumu kwa zaidi ya miaka saba sasa.

Katika taarifa yake kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa hii leo kuhusu Syria, Bi. Mueller amesema mgogoro huo umesababisha mateso makubwa  kwa wananchi, vifo vingi kwa raia na huku wengine wakijeruhiwa au kutojulikana waliko.

Ukatili dhidi ya wakawake marufuku Burundi: Seruka

Ukatili wa kijinsia ni changamoto kubwa nchini Burundi huku Zaidi ya asilimia 90 ya wanaotendewa ukatili huo wakiwa ni wanawake na watoto. Sasa shirika lisilo la kiserikali la SERUKA limeamua kushikia bango dhuluma hiyo kwa kuendesha kampeni katika maeneo mbalimbali nchini humo kupinga na kuelimisha jamii kuachana na ukatili dhidi ya wanawake. Mwandishi wetu wa maziwa makuu Ramadhan Kibuga alitembelea moja ya kampeni za shirika hilo kwenye uwanja wa Parke mjini Bujumbura uangana naye kwenye Makala hii.

Habari za UN- Mtazamo wa kimataifa; Habari za kiutu

Kunani?

Wavuti wa Radio ya Umoja wa Mataifa unafungwa rasmi mwishoni mwa mwezi Januari 2018. Nafasi yake itachukuliwa na ukurasa mpya ambao tuna imani utawapatia wasikilizaji na washirika katika vituo mbali mbali vya radio duniani, taarifa bora zaidi katika muundo tofauti.

Idara ya Habari kwa Umma ya Umoja wa Mataifa inayo furaha kuzindua wavuti huo ambamo kwao utapata taarifa katika mifumo yote. Mabadiliko haya kutoka Radio ya Umoja wa Mataifa hadi Habari za UN ni matokeo ya tafiti za kina kuhusu matumizi na mahitaji ya hadhira yetu.

Watu millioni 2.7 bado wakabiliwa na njaa kali Somalia

Uzalishaji wa chakula pamoja na vyanzo vya mapato vingi nchini Somalia vinatarajiwa kusalia chini kuliko kawaida  katika maeneo mengi nchini humo.

Hii ni kutokana  na uhaba mkubwa wa mvua za msimu za Oktoba- Disemba mwaka 2017 katika maeneo mengi ya Somalia huku mvua za msimu wa April hadi Juni  zikitabiriwa nazo kuwa za kiwango cha chini.

Mvua zinazosaidia uzalishaji chakula nchini humo ni za aina mbili  Deyr na Ga. Msimu wa Deyr hutokea katika miezi ya Oktoba hadi Disemba kila mwaka na  ule wa Ga unaanza  Aprili hadi Juni kila mwaka.

Hema linalohimili mabadiliko ya tabia nchi ni nuru kwa wakimbizi Uganda

Wakimbizi wa Sudani Kusini waishio kwenye makazi ya wakimbizi ya Maaji -Adjuman kaskazini mwa Uganda sasa wananeemeka na huduma ya afya kupitia hema maalumu linalohimili mabadiliko ya tabia nchi. Hema hilo la aina yake duniani limetolewa kama zawadi kwa wakimbizi hao na wanafunzi wa chuo kikuu cha Makerere baada ya hema hilo kuwawezesha kushinda tuzo ya ubunifu wa kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi. Kwa maelezo zaidi tuungane na Siraj kalyango

Photo: UNCTAD

Mabilioni yapotea kwa kutotumia vizuri mikataba ya biashara huru, FTAs

Ripoti mpya iliyotolewa leo imeonyesha kuwa bado kuna shida kubwa katika matumizi sahihi ya mikataba ya biashara huria ambayo Muungano wa Ulaya imetia saini na nchi zingine.

Matumizi yasiyotosheleza ya mikataba hiyo husababisha kupotea kwa dola takribani bilioni 89, imesema ripoti hiyo iliandaliwa kwa pamoja na kamati ya biashara na maendeleo ya Umoja wa Mataifa, UNCTAD na bodi ya taifa ya biashara ya Sweden.

Katu hatutokubali utumwa urejee Afrika- Guterres

Mkutano wa kawaida wa 30 wa viongozi wa Afrika ukiendelea huko Addis Ababa, Ethiopia, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametaja mambo matano ya kuimarisha ushirikiano kati a pande mbili hizo.

Akihutubia wakati wa ufunguzi wa kikao hicho, Bwana Guterres ametaja mambo hayo kuwa ni amani na usalama, uhamiaji, maendeleo endelevu, mabadiliko ya tabianchi na vita dhidi ya rushwa.

Akizungumzia  uhamiaji,  Katibu Mkuu amerejelea masikitiko yake kuhusu utumwa wa kisasa wakati huu ambapo visa vya utumwa vimeripotiwa huko Libya hivyo amesema..