Kutana na binti kutoka Uganda, Christine Joyce ambaye anasema asilani hatolisahau janga la corona au COVID-19 ambalo mbali ya kumnyima masomo wakati wa sheria za kusalia majumbani limechangia kumwacha na kilema cha maisha. Hata hivyo amesema hatokata tamaa ya kutimiza ndoto yake ya kuendelea na masomo na hatimaye siku moja kuwa daktari.