Kimbunga Melissa ni tishio Carribea ,watoto milioni 1.6 wako hatari: UNICEF
Wakati Kimbunga Melissa kikitarajiwa kuleta mvua kubwa na upepo mkali katika eneo la Carribea, takriban watoto milioni 1.6 wako hatarini, huku familia katika nchi za Jamaica, Haiti na visiwa jirani zikijiandaa kwa mafuriko, maporomoko ya ardhi na uharibifu mkubwa kwa mujibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto UNICEF.