Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

watoto

UNICEF/James Ekwam

Msaada wa UNICEF waokoa manusura wa mafuriko Magharibi mwa Kenya

Kupitia  msaada wa fedha kutoka Ufaransa, juhudi za kuboresha hali ya lishe kwa watoto nchini Kenya, hasa kwa jamii zilizo katika mazingira hatarishi zinaendelea ambapo juhudi za hivi karibuni ni kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) kwa kushirikiana na Shirika la Msalaba Mwekundu la Kenya ambao kwa pamoja wameimarisha huduma hizo kwa manusura wa mafuriko Magharibi mwa taifa hilo la Afrika Mashariki. Huduma hizi ni sehemu muhimu ya kuhakikisha watoto na familia wanapata vyakula vyenye virutubishi kwa ustawi wa maisha yao.

Sauti
3'10"
Beatrice Nabwire Okumu kutoka Busia akiwa na mtoto wake nje ya hema lao baada ya kukumbwa na mafuriko. Yeye ni mnufaika wa msaada wa lishe kutoka UNICEF Kenya.
© UNICEF

UNICEF yasaidia manusura wa mafuriko Magharibi mwa Kenya

Kupitia  msaada wa fedha kutoka Ufaransa, juhudi za kuboresha hali ya lishe kwa watoto nchini Kenya, hasa kwa jamii zilizo katika mazingira hatarishi zinaendelea ambapo juhudi za hivi karibuni ni kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) kwa kushirikiana na Shirika la Msalaba Mwekundu la Kenya ambao kwa pamoja wameimarisha huduma hizo kwa manusura wa mafuriko Magharibi mwa taifa hilo la Afrika Mashariki. Huduma hizi ni sehemu muhimu ya kuhakikisha watoto na familia wanapata vyakula vyenye virutubishi kwa ustawi wa maisha yao.

Sauti
3'10"

09 OKTOBA 2025

Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayoangazia siku ya posta Duniani na tunakupeleka nchini Tanzania ambako huko Sabrina Said wa idhaa hii amefuatilia harakati za huduma hiyo kwenye shirika la Posta Tanzania lililoanzishwa kwa sheria ya Bunge ya mwaka 1993 na kuanza kutoa huduma Januari 1994.

Sauti
11'21"
© UNRWA

Gaza: Mashirika ya UN yaonya kuwa hospitali zimegeuka kuwa uwanja wa mapambano

Umoja wa Mataifa umeonya kuwa hali ya kibinadamu katika Ukanda wa Gaza imefikia hatua ya kutisha, huku hospitali zikigeuzwa kuwa uwanja wa mapambano, kukizidiwa na wagonjwa na misaada kukwama. Maafisa wa Umoja wa Mataifa wameaambia waandishi wa habari leo mjini Geneva kuwa kuwa watoto wanakosa hewa ya oksijeni, wagonjwa wanakufa kwenye meza za upasuaji, na risasi zinavurumishwa moja kwa moja ndani ya hospitali.  Flora Nducha amefuatilia na hii hapa taarifa yake

Sauti
2'58"
© UNICEF/Eyad El Baba

Amri ya kuhama 'kaa la moto' kwa WaPalestina Gaza

Baada ya amri iliyotolewa na jeshi la Israel la kuwataka Wapalestina walioko katika eneo la mji wa Gaza huko Ukanda wa Gaza eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israel kuondoka eneo hilo kwani linataka kufanya mashambulizi, hali imekuwa mbaya kwa wananchi hususan wazee ambao sasa wanafunga safari kilometa nyingi kuondoka eneo hilo. Leah Mushi anatujuza masahibu wanayo kumbana nao watu hao.

Sauti
3'2"
Wanawake wakijifunza kusoma na kuandika kupitia mpango wa Umoja wa Mataifa unaoungwa mkono na Wanawake wa kusoma na kuandika katika jimbo la Nuristan, mashariki mwa Afghanistan.
© UN Women/Sayed Habib Bidell

Miaka minne ya kunyima elimu wasichana wa Afghanistan ni “Moja ya uonevu mkubwa wa wakati wetu” - UNICEF

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, UNICEF, Catherine Russell, ametahadharisha vikali kuhusu marufuku inayoendelea ambayo imewazuia kwa kipindi cha miaka minne sasa wasichana balehe nchini Afghanistan kuhudhuria shule akiiita “tishio kubwa” kwa mustakabali wa taifa hilo.

Sauti
2'42"