Chuja:

Redio ya UM

Uwazi utasaidia kuondoa shuku juu ya silaha za maangamizi- Guterres

Tishio la matumizi ya silaha za maangamizi linaongezeka kila uchao licha ya juhudi za kimataifa za kudhibiti na hatimaye kutokomeza matumizi ya silaha hizo.

Amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres wakati akihutubia kikao cha ngazi ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kilichofanyika leo New York, Marekani kuangazia mbinu za kujengeana imani ili kuondoa silaha hizo.

Guterres amesema dunia hivi sasa ina wasiwasi kuwa penginepo silaha za nyuklia zinaweza kutumiwa, hofu ambayo iko kiwango cha juu zaidi tangu kumalizika kwa vita baridi.

Waasi Colombia washambulia bomba la mafuta

Nchini Colombia, mashambulio ya bomu yameripotiwa hii leo kwenye bomba la kusafirisha mafuta la Cano Limon katika majimbo ya Arauca na Boyaca, ikiwa ni siku moja tu baada ya kumalizika kwa muda wa makubaliano ya muda ya kusitisha mapigano kati ya serikali na kikundi cha National Liberation Army, ELN.

Mikopo yahatarisha maisha ya wakimbizi wa Syria huko Lebanon

Maisha ya wakimbizi wa Syria waliokosaka hifadhi Lebanon yanazidi kuwa hatarini kila uchao, wakati huu ambapo zaidi ya nusu yao ni mafukara.

Hiyo ni kwa mujibu wa mashirika ya Umoja wa Mataifa ikiwemo lile la wakimbizi, UNHCR, la watoto, UNICEF na lile la mpango wa chakula WFP.

Mashirika hayo kupitia utafiti wao yamesema miaka saba ya vita nchini Syria imefanya raia wengi kushindwa kukidhi mahitaji ya maisha yao na baya zaidi ni wategemezi kwa misaada ya kimataifa ambayo nayo haina uhakika.

Choo chako ni salama?

Utafiti umebaini kwamba ukosefu wa vyoo safi  na salama ni hatarishi kwa afya ya binadamu. Takwimu za mashirika ya ufya ulimwenguni kama WHO na wengine zinaonyesha kuwa jamii zinazoishi katika mazingira yasiyo na vyoo salama zipo katika athari za kupatwa na milipuko ya magonjwa yatokanayo ya ukosefu wa matumizi salama ya vyoo kama kipindupindu na magonjwa mengine.