Mkutano wa mwaka wa kamisheni ya Umoja wa Mataifa kwa Afrika, ECA ukiendelea huko Kigali, Rwanda kwa kuangazia utekelezaji wa makubaliano ya eneo huru la biashara barani Afrika, AfCFTA, Kenya imezungumzia sababu za kupatia kipaumbele eneo hilo huru la biashara.