COVID-19 na athari zake kwa mazingira hasa maeneo ya mbugani
Pakua
Nchini Tanzania harakati za utalii tena siyo tu wa raia wa ndani, bali pia wageni kutoka nje ya nchi, zilirejea mwezi Juni mwaka huu baada ya kusitishwa kwa muda kutokana na janga la ugonjwa wa Corona au COVID-19 ulioripotiwa nchini humo mwezi Machi mwaka huu.
Sasa hali imerejea kawaida na watalii wanaendelea kutembelea vivutio mbalimbali. Hata hivyo awali ugonjwa huo ulikuwa na athari kwenye maeneo ya mbugani ni kwa vipi? Stella Vuzo amezungumza na afisa wa shirika la mpango wa maendeleo la Umoja wa Mataifa, UNDP ambalo huwa linasaidia harakati za uhifadhi wa mazingira nchini Tanzania.
Audio Credit
UNIC DAR/Stella Vuzo
Audio Duration
3'36"