Vita ya Urusi na Ukraine imevuruga uchumi wangu – Abeid Aboubakar wa Dodoma, Tanzania
Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres hivi karibuni akizungumza na Baraza la Usalama alitaka hatua zichukuliwe kukomesha vita alipokuwa akizungumzia namna ambavyo ni vita ni chachu kubwa ya njaa duniani kote.
Vita ya hivi karibuni ambayo imeongeza chumvi katika jeraha ni kutokana na uvamizi wa Urusi kwa Ukraine ambao pamoja na madhara mengine kwa ulimwengu, imeathiri uzalishaji na usambazaji wa mafuta ambayo ni bidhaa mtambuka kwa mambo mengi na inapoyumba inayumbisha karibu mihimili yote ya uchumi.