Mradi wa UNEP wa kutunza ardhioevu waanza kutekelezwa Zambia
Serikali ya Zambia inatekeleza mradi mpya wa miaka minne wa kusaidia jamii karibu na ardhi oevu ya Lukanga na Bangweulu katika majimbo ya Kati na Luapula nchini humo.
Serikali ya Zambia inatekeleza mradi mpya wa miaka minne wa kusaidia jamii karibu na ardhi oevu ya Lukanga na Bangweulu katika majimbo ya Kati na Luapula nchini humo.
Harakati za kuvunja makundi yaliyojihami nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC na hatimaye askari wake kujumuishwa kwenye jamii zinaendelea kama njia mojawapo ya kusongesha amani na kupata amani ya kudumu huko upande wa mashariki mwa taifa hilo la Maziwa Makuu barani Afrika.
Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, hali ngumu ya maisha inatumbukiza vijana katika mapigano ya msituni mashariki mwa taifa hilo la Maziwa Makuu. Kwa kubaini hilo, Umoja wa Mataifa kupitia ujumbe wake wa kulinda amani nchini humo MONUSCO unatekeleza miradi kama ule wa kuvunja makundi yaliyojihami, kupokonya silaha wanamgambo na kuwajumuisha kwenye jamii, DDR, mradi ambao unatamatishwa kwa kuwapatia wapiganaji hao wa zamani stadi za maisha ili wajipatie kipato.
Baionuai ni muhimu sana katika sayari ya dunia ili kuhakikisha usitawi na maisha ya viumbe hai kama vile binadamu, wanyama, ndege, mimea na wadudu kwa namna nyingi. Mimea nayo husafisha hewa chafu na kuzalisha oksijeni.
Pamoja na uwepo wa lengo namba tano la Umoja wa Mataifa linalosisitiza kupatikana haki sawa kwa jinsia zote, hali bado ni tofauti hasa katika sekta ya ardhi na kilimo. Mfano halisi ukiwa katika maeneo mengi barani Afrika amba wanawake wanaendelea kuwa waathirika wa mfumo dume kandamizi unaowafanya kukosa haki ya kumiliki ardhi.
Mbali na janga la Janga la Corona au COVID-19 ambalo limeikumba dunia kwa zaidi ya miaka miwili, wananchi wa Uganda waishio karibu na Ziwa Albert kwa miaka hiyo miwili wamekuwa wakikabiliwa na changamoto ya ziada ya mafuriko.
Wanawake wanachama wa kikundi cha Kaizo Women’s Group (KWG) wilayani Hoima ni moja wapo ya vikundi ambayo mipango yao ilikwamishwa na atahri za mafuriko na ambao sasa wanaomba msaada wa kifedha kutoka serikali katika juhudi zao za kujikwamua kutokana na uharibifu wa maji huku wakikabiliana na janga la COVID-19.
katika kukuza lugha ya Kiswahili duniani Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania BAKITA limeandaa kongamano la wiki moja la Idhaa za Kiswahili duniani na kuwakutanisha wadau kutoka nchi mbalimbali zinazozungumza lugha ya Kiswahili jijini Arusha nchini humo.
Janga la Corona au COVID-19 lilipoibuka miaka miwili iliyopita halikuleta changamoto za afya pekee bali kiuchumu na masuala mengine ya kijamii kama hofu juu ya taarifa zihusianazo na janga hilo. Kwakuwa janga hilo lilikuwa jipya wananchi wengi walijikuta wakihamaki kutokana na kuenea kwa taarifa za uzushi zilizokuwa zikisambaa mitandaoni.
Miradi mbalimbali inayotekelezwa na mashirika ya Umoja wa Mataifa na wadau wake kote duniani, imeweka wazi ukweli kwamba vikwazo mbalimbali vinavyowakabili wanawake vinapoondolewa, wanawake wanakuwa chachu ya kuleta mabadiliko chanya katika karibia kila sekta katika jamii.