Sawa Wanawake Tanzania yakabidhi majengo mawili kwa serikali ya Tanzania kusaidia vita dhidi ya unyanyasaji wa watoto
Mwishoni mwa mwaka jana 2021, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF lilisema mwaka huo ulikuwa wa machungu na ukiukwaji mkubwa wa haki za watoto. Ingawa taarifa ya UNICEF ililenga katika mizozo ya muda mrefu na ile mipya ni wazi kuwa matukio ya ukiukwaji wa haki za watoto na unyanyasaji dhidi yao, unaendelea kujidhihirisha katika maeneo mbalimbali duniani.