Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala

Picha: UN News

Lengo la ujumuishi kwenye elimu na kutomwacha mtu yeyote nyuma ladhihirika Tanzania

Umoja wa Mataifa unatambua kuwa elimu ina uwezo mkubwa wa kumuinua mtu kiuchumi na kijamii, kwa maana ya kwamba ni silaha mujarabu ya kuondokana na umaskini. Kupitai malengo ya maendeleo endelevu, SDGs, hususan lengo namba 4, Umoja wa Mataifa unataka elimu bora tena isiyomwacha mtu yeyote nyuma, kwa misingi ya rangi, eneo aliko au hali ya mwili wake. Tayari nchi na mashirika ya kimataifa na yasiyo ya kiserikali yanafanikisha lengo hilo, mfano humo nchini Tanzania katika mkoa wa Morogoro ulioko mashariki mwa taifa hilo la Afrika. 

Sauti
5'3"
UN News

Mradi wa PLEAD wawezesha huduma za mahamaka kupatikana muda wote nchini Kenya

Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya madawa na uhalifu UNDOC kanda ya Afrika Mashariki kwa kushirikiana na sekta ya mahakama nchini kenya wamepanga kuanza kutekeleza awamu ya pili ya mradi wa uwekaji umeme wa sola katika mahakama na magereza nchini humo baada ya awamu ya kwanza kuonesha mafanikio.

Kupitia mradi ujulikanao kama PLEAD unaofadhiliwa na Muungano wa Ulaya UNODC na sekta ya mahakama nchini Kenya wamefanikiwa kutekeleza mradi wa awamu ya kwanza katika mahakama mbili zilizoko Mombasa ambazo zilikuwa zikishindwa kuendesha shughuli zake pindi umeme unapokatika.

Sauti
3'23"
IAEA Video

Teknolojia ya nyuklia yaleta matumaini kwa wakulima nchini Kenya

Je ni kwa vipi teknolojia ya nyuklia inaweza kuleta tofauti katika uzalishaji wa chakula wakati huu ambapo janga la tabianchi linazidi kugonga vichwa vya watu na kubisha hodi kila uchao? Baadhi ya watu wakisikia nyuklia kinachowajia kichwani ni mabomu ya nyuklia, lakini nchini Kenya, wanasayansi na wakulima wanaelezea kwa maneno yao wenyewe vile ambavyo sayansi ya nyuklia inasaidia kupambana na uhaba wa chakula na maji. Kuanzia uzalishaji wa mbegu mpya zinazohimili ukame hadi teknolojia za kutambua ni muda gani muafaka kumwagilia mazao.

Sauti
4'43"
UNHCR Video

Mkimbizi aliyerejea nyumbani Burundi kutoka Tanzania awaambia wenzake, "rejeeni nyumbani tujenge nchi yetu."

Akiwa katika ziara yake ya kwanza nchini Burundi hivi karibuni, Naibu Kamishna Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi duniani, UNHCR Kelly Clements ameihi jamii ya kimataifa iongeze msaada kwa maeneo na jamii ambako wakimbizi wa Burundi wameamua kurejea nyumbani kwa hiari. 

Tangu mwaka 2017, zaidi ya wakimbizi 200,000 wa Burundi wamerejea nyumbani kutoka nchi jirani kama vile Tanzania. 

Sauti
3'52"
IFAD

Wakulima wenye ulemavu nao wanaweza kujipatia kipato

Inakadiriwa kuwa asilimia 20 ya watu maskini zaidi duniani wana aina fulani ya ulemavu. Watu wa vijijini wanaoishi na ulemavu wanakabiliwa na changamoto zaidi kuliko wenzao wa mijini ndio maana ushirikishwaji wa watu wenye ulemavu ni lengo muhimu katika kutekeleza azma ya Mfuko wa umoja wa Mataifa wa Maendeleo ya Kilimo, IFAD. 

IFAD tayari ina uzoefu katika kufanya kazi na watu wenye ulemavu. Katika miaka ya hivi karibuni, IFAD imekuwa ikiongeza juhudi zake za kuwajumuisha watu wote wenye ulemavu. 

Sauti
3'53"
UNICEF/van Oorsouw

Jamii inaelewa nini kuhusu ukatili wa kijinsia

Kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya wanawake, UN Women ukatili dhidi ya wanawake na wasichan unasalia kuwa kitendo cha ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu duniani kote, ukiathiri zaidi ya wanawake milioni 1.3, takwimu ambayo hata hivyo haijabadilika kwa zaidi ya muongo mmoja

Sauti
3'46"
UN Women

Girl Shine ya UN Women imenijengea kujiamini na sasa nasaidia familia yangu- Rachael

Mizozo na umaskini wa kupindukia kwenye mazingira ya uhitaji mkubwa wa msaada wa kibinadamu huwaweka wasichana katika hatari kubwa ya kukumbwa na ukatili na kunyanyaswa. Shirika la Umoja wa Mataifa la kushughulikia masuala ya wanawake, UN WOMEN kwa kutambua hilo linatekeleza miradi katika kambi za wakimbizi za Dadaab na Kakuma nchini Kenya ili kuwajengea uwezo wasichana barubaru ili hatimaye waweza kuandaa mustakabali bora wa maisha yao. Girls Shine ni moja ya miradi hiyo kupitia mradi mkubwa wa LEAP unaoungwa mkono na serikali ya Japan tangu mwaka 2018.

Sauti
3'13"