Taasisi ya PGWOCADE na harakati za kumkomboa msichana mkoani Rukwa Tanzania.
Mojawapo ya vikwazo vya harakati za kumwinua mwanamke kutoka katika hali duni iliyodumu tangu enzi na enzi mila na desturi za baadhi ya maeneo duniani ambayo wanajamii wamekwenda kwa kasi ndogo katika kuziacha mila hizo kandamizi na potofu. Licha ya ugumu huo, bado mazingira hayo hayapaswi kuwa kikwazo kwa wanarahakati ambao wanahaha kufikia usawa wa kijinsia kwani mabadiliko ya mila na desturi hayawezi kuwa ya siku moja.