Afrika yapazia sauti mambo 6 COP25
Wakati mkutano huo wa COP25 ukiendelea mashirika ya asasi za kiraia kutoka barani Afrika yakiwakilisha nchi zaidi ya 40, chini ya mwamvuli wa Muungano wa Afrika wa haki na tabianchi (PACJA), yamedai jumuiya ya kimataifa kuchapuza mchakato na maamuzi yatakayozingatia mazingira na maslahi ya bara hilo .