Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ni sisi wanawake tutakaoubadilisha msemo wa adui wa mwanamke ni mwanamke-Jonitha Nitoya Joram

Ni sisi wanawake tutakaoubadilisha msemo wa adui wa mwanamke ni mwanamke-Jonitha Nitoya Joram

Pakua

Mabadiliko chanya katika jamii yanaweza kuanzishwa na mtu mmoja tu, hiyo ndiyo imani ya msichana Jonitha Nitoya Joram muhitimu wa Chuo Kikuu ambaye ameamua kuutumia muda wake wa ziada kuwaelimisha wasichana wenzake na wanawake wafanyabiashara nchini Tanzania ambao hawana elimu ya ujasiriamali. Joanitha anatoa wito kwa kila mtu katika jamii kusambaza kwa upendo maarifa aliyonayo ili kuweza kumkomboa kila mmoja katika jamii hususani wale ambao hawakujaliwa kuipata elimu. Arnold Kayanda wa UN News amefanya mahojiano na msichana huyu anayeanza kwa kueleza namna alivyoanza harakati hizo.

Audio Duration
3'33"
Photo Credit
UN News