Harakati za kupinga ukatili dhidi ya wanawake kwenye maeneo ya migodi Uganda zashika kasi
Pakua
Siku 16 za kimataifa za kupinga ukatili dhidi ya wanawake na wasichana zikiendelea kuangaziwa duniani, ni wazi kuwa ukatili wa kijinsia ni changamoto ya ulimwenggu ukiwa na madhara makubwa kwa watoto wa kike na wanawake. Nchini Uganda uzinduzi wa filamu itwayo ‘Wanawake Hushikilia Anga’ ni miongoni mwa harakati za asasi za kiraia zilizofanyika nchini humo katika uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia. Je nini kimefanyika, ungana basi na John Kibego katika, ambaye amekuwa shuhuda wetu.
Audio Credit
Flora Nducha/John Kibego
Audio Duration
3'32"