Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Jarida la Habari

08 Februari 2021

Hii leo jaridani ni mada kwa kina ambapo Grace Kaneiya kutoka Nairobi Kenya anaangazia wanufaika wa mradi wa shirika la chakula na kilimo la Umoja wa Mataifa, FAO nchini Tanzania katika kuwezesha wakulima mkoani Kigoma kulima maharagwe aina ya Jesca yenye virutubisho. N katika kuelekea siku ya kimataifa ya mikunde tarehe 10 mwezi Februari mwaka huu. Habari kwa ufupi tunaangazia India na maporomoko ya theluji, harakati za kukabili kuenea kwa Ebola iliyotangazwa kuibuka tena Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC na mashinani anabisha hodi Lebanon akimulika pia harakati za FAO. Karibu!

Sauti
11'11"

05 Februari 2021

Leo Ijumaa ni mada kwa kina na Assumpta Massoi anakupeleka Nairobi Kenya ambako Grace Kaneiya katika kufuatilia utekelezaji wa mwaka wa kimataifa wa mboga mboga na matunda amevinjari kwa familia moja jijini Nairobi kuona mtazamo wao katika ulaji wa mboga za majani na matunda.

Sauti
10'39"

04 Februari 2021

Hii leo jaridani Grace  Kaneiya kutoka Nairobi nchini Kenya anaanzia na taarifa kuhusu siku ya saratani duniani ikimulika changamoto za upimaji wa gonjwa hilo wakati huu wa janga la COVID-19. Kisha anakwenda Morogoro nchini Tanzania kumulika tatizo la lishe duni na makuzi ya mtoto, halafu anakupeleka Jamhuri ya Afrika ya Kati ambako amani imerejea katika mji wa Bangassou uliokuwa kitovu cha mashambulizi tarehe 3 mwezi uliopita.

Sauti
13'25"

03 Februari 2021

Leo Jumatano Flora Nducha anaanzia huko Madagascar ambako ukame wa muda mrefu umesababisha njaa kali na watu kulazimika kutengeneza rojo la ukwaju na kunywa huku wakilumangia na udongo mweupe. Kisha anakwenda Tigray nchini Ethiopia ambako nako hali si hali kwa wakimbizi wa ndani wakimbiao mapigano na wale waliotoka Eritrea. Hata hivyo WFP ambalo ni shirika la mpango wa chakula la Umoja wa Mataifa  limetangaza mpango wake wa kusambaza kwa haraka chakula kwa wenye uhitaji zaidi barani Afrika.

Sauti
15'7"

02 Februari 2021

Hii leo jaridani Flora Nducha anaanza na ripoti ya Umoja wa Mataifa kuhusu usafirishaji haramu wa binadamu ikionesha kuwa wavulana wanaosafirishwa kiharamu idadi yao imeongezeka katika kipindi cha miaka miwili iliyopita. Watu wengine wanasafirishwa pia kutumikishwa kwenye kuombaomba. Kisha atakufikisha Baidoa nchini Somalia kumulika hali ya kibinadamu na hatimaye Sudan Kusini ambako shule moja ya sekondari yaonesha uwezo wa wanafunzi wakimbizi.

Sauti
13'59"

01 Februari 2021

Hii leo jaridani tunammulika Noela Kombe, al maarufu Mamaa Noela kutoka kule Beni jimboni Kivu Kaskazini na jinsi anavyotekeleza wito wake wa kusaidia watoto yatima. Hiyo ni katika mada kwa kina lakini kuna muhtasari wa habari tukianzia Somalia, kisha Myanmar na hatimaye Sudan Kusini. Mashinani tunabisha hodi leo shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO, ambako daktari anazungumzia suala la ugonjwa wa Corona au COVID-19 barani Afrika. Karibu na mwenyeji wako ni Flora Nducha.

Sauti
10'45"

29 Januari 2021

Hii leo Ijumaa ni mada kwa kina , leo tutaelekea Nairobi, mji mkuu wa Kenya ambapo tutakutana na mfanyakazi wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR Wanja Munaita akielezea jinsi alivyoweza kutimiza ndoto yake kuanzia kusaidiwa na shirika hilo hadi yeye kusaidia wengine kupitia shirika hilo. Kuna habari kwa ufupi tukimulika ghasia Darfur, Sudan halikadhalika CAR na pia neno la wiki leo ni maana ya Ugua Pole! Karibu na mwenyeji wako ni Flora Nducha.

Sauti
10'45"

28 Januari 2021

Hii leo jaridani Flora Nducha anaanza na vipaumbele vya mwaka huu wa 2021 vya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ambavyo ni 10. Kisha anakwenda Tanzania kutamatisha sehemu ya pili ya taarifa kuhusu jinsi mashirika ya Umoja wa Mataifa yameleta kujiamini kwa wasichana Angel na Fatma. Kisha anabisha hodi huko Mediteranea ambako twaelezwa kuwa janga la tabianchi ukanda wa Sahel na ghasia pembe ya Afrika vyazidi kusukuma watu kusaka mbinu zote kuvuka baharí na kwenda Ulaya. Makala tunamaliza sehemu ya pili kutoka kwa Mzee Peter Semiga wa Uganda na pia kuna mashinani. Karibu!

Sauti
14'3"

27 Januari 2021

Hii leo jaridani Flora Nducha anaanzia nchini Tanzania kumulika harakati za watoto wa kike na elimu, kisha anakukutanisha na wajasiriamali vijana kupitia shirika la maendeleo ya viwanda la Umoja wa Mataifa, UNIDO. Baada ya hapo anakupeleka Vietnam ambako utaalamu umemaliza tabia ya wakulima kuonja maji ili kutambua iwapo yana chumvi nyingi au la kabla ya kumwagilia kwenye mpunga. Makala tunakwenda Nairobi nchini Kenya ambako kijana aliyekuwa sugu mtaani sasa amegeuka mkombozi kwa vijana wengine waliokuwa tishio mitaani na anatamatisha na mashinani kutoka Sudan Kusini, karibu!

Sauti
13'43"

26 Januari 2021

Hii leo jaridani Flora Nducha anaanzia Msumbiji ambako kimbunga Eloise kimetonesha kidonda cha manusura wa vimbunga Chalane na Idai. Kisha atabisha hodi Burkina Faso akimulika raia waliokimbia vurugu makwao wakikumbwa na janga la mabadiliko ya tabianchi. Anabisha hodi pia Somalia ambako mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametembelea jimbo la Galmudug. Makala tunakwenda kaunti ya Nakuru nchini Kenya kukukutanisha na Bibi Afya na mashinani tunasalia huko huko kusikia jinsi skauti wa Kenya wameamka sasa wanalinda mazingira. Karibu! 

Sauti
13'6"