Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

26 Januari 2021

26 Januari 2021

Pakua

Hii leo jaridani Flora Nducha anaanzia Msumbiji ambako kimbunga Eloise kimetonesha kidonda cha manusura wa vimbunga Chalane na Idai. Kisha atabisha hodi Burkina Faso akimulika raia waliokimbia vurugu makwao wakikumbwa na janga la mabadiliko ya tabianchi. Anabisha hodi pia Somalia ambako mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametembelea jimbo la Galmudug. Makala tunakwenda kaunti ya Nakuru nchini Kenya kukukutanisha na Bibi Afya na mashinani tunasalia huko huko kusikia jinsi skauti wa Kenya wameamka sasa wanalinda mazingira. Karibu! 

Audio Credit
Flora Nducha
Audio Duration
13'6"