23 Februari 2022
Karibu kusikiliza jarida ambapo leo tutakuletea mada kwa kina kutoka viziwani Zanzibar nchini Tanzania , ambapo ikiwa imesalia chini ya miaka 8 kufikia ukomo wa malengo ya amendeleo endelevu SDG’s juhudi zinafanyika kwa hali na mali kuhakikisha jamii zinafikia malengo hayo. Miongoni mwa wanaharakati wa kupigia upatu malengo hayo ni mke wa Rais wa serikali ya mapinduzi ya Zanzibar Bi. Mariam Mwinyi ambaye mwishoni mwa wiki amezindua wakfu au taasisi maalum ijulikanayo kama “Zanzibar Maisha Bora Foundation”.