17 Februari 2020
Hii leo jaridani Assumpta Massoi anaanzia nchini Kenya ambako Umoja wa Mataifa umeanza kupatia mafunzo vijana 300 wa jeshi la huduma kwa vijana kwa lengo la kusaidia kudhibiti nzige wa jangwani waliovamia taifa hilo tangu mwezi Desemba mwaka jana. Kisha anakwenda Sudan Kusini ambako walinda amani wa Umoja wa Mataifa wamekarabati na kushehenisha vitabu kwenye maktaba ya watoto mjini Juba.