Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Jarida la Habari

17 Februari 2020

Hii leo jaridani Assumpta Massoi anaanzia nchini Kenya ambako Umoja wa Mataifa umeanza kupatia mafunzo vijana 300 wa jeshi la huduma kwa vijana kwa lengo la kusaidia kudhibiti nzige wa jangwani waliovamia taifa hilo tangu mwezi Desemba mwaka jana. Kisha anakwenda Sudan Kusini ambako walinda amani wa Umoja wa Mataifa wamekarabati na kushehenisha vitabu kwenye maktaba ya watoto mjini Juba.

Sauti
12'20"

14 FEBRUARI 2020

Leo siku ya wapendanao Duniani katika Jarida la Habari la Umoja wa Mataifa Anold Kayanda anakuletea

-Wahamiaji 11,500 walikwenda Yemen kila mwezi kutoka Pembe ya afrika mwaka jana limesema shirika la Umoja wa Mataifa la uhamiaji IOM

-WFP inaendelea kutoa msaada wa chakula cha dharura kwa watu ambao wako katika uhitaji mkubwa kaskazini magharibi mwa Syria licha ya uhasama ulioongezeka ambao wiki hii ulisababisha kusimamisha usambazaji wa misaada kwa saa 24. 

Sauti
10'43"

13 FEBRUARI 2020

Katika Jarida la Habari la Umoja wa Mataifa hii leo Arnold Kayanda anakuletea

-Umoja wa Mataifa umesema Redio inasalia kuwa chombo muhimu cha kuunganisha jamii na kuchangia katika kusongesha mbele ajenda ya maendeleo endelevu SDG's

-Katika kuadhimisha siku ya Radio Duniani ambayo kila mwaka hufanyika Februari 13, shirika la Umoja wa Mataifa la elimu sayansi na utamaduni UNESCO limesema Redio ndio chombo cha mawasiliano cha kesho lazima ienziwe

Sauti
10'45"

12 FEBRUARI 2020

Katika Jarida la Habari hii leo anold Kayanda kutoka Umoja wa Mataifa anakuletea

-Shirika la afya ulimwenguni WHO leo limetoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kutousahau ugonjwa wa Ebola pamoja na kwamba inakabiliana na virusi vya Corona hivi sasa kwani kufanya hiyo itakuwa kosa la jinai lenye madhara makubwa ya kibinadamu

-Mradi wa UNICEF wa mafunzo kwa waendesha boda boda ni nuru kwa wanawake wajawazito na watoto wagonjwa nchini Uganda

Sauti
11'36"

07 FEBRUARI 2020

Jaridani Februari 07, 2020 na Anold Kayanda. Ikiwa leo ni Ijumaa utasikia Habari kwa ufupi, mada kwa kina imejikita katika suala la ukeketaji tukiangazia nchini Tanzania ambako manusura mmoja anapambana kuhakikisha hakuna mtoto mwingine wa kike atakayekumbana na madhila haya. Na ikiwa leo ni Ijumaa tutasikia uchambuzi wa methali la wiki kutoka BAKIZA.

Sauti
10'23"

06 Februari 2020

Ukeketaji unaathiri wasichana na wanawake na gharama ya matibabu ni dola bilioni 1.4 kwa mwaka kimataifa imesema WHO, Mwaka mmoja baada ya makubaliano ya amani, mamilioni ya watoto CAR bado wako hatarini. Tangu nimeacha ungariba nimeshawaokoa wato takribani 150-Aliyeacha ungariba.

Sauti
10'15"

05 FEBRUARI 2020

Katika Jarida la Habari hii leo kutoka Umoja wa Mataifa Anold Kayanda anakuletea
-UNHCR yaongeza hatua za kukabiliana na hali ya wakimbizi Sahel ghasia zikishika kasi
-Somalia inahitaji msaada wa kibinadamu wakati watu milioni 4.1 wakikabiliwa na kutokuwa na uhakika wa chakula
-UNESCO yasema asilimia 32 ya watu wa zaidi ya miaka 15 Nepali hawajui kusoma wala kuandika
-Makala yetu leo inatupeleka mkoani Kagera kumulika mchango wa wauguzi na wakunga
Na Mashinani tuko Afghanistan ambako UNICEF inapambana na utapiamlo

Audio Duration
11'41"

04 FEBRUARI 2020

Katika Jarida la Habari hii leo kutoka Umoja wa Mataifa arnold Kayanda anakuletea
-Shirika la afya ulimwenguni WHO limetaja hatua za kunusu maisha ya watu milioni 7 kutokana na saratani
-Watu zaidi ya 520,000 wamefurushwa makwao Syria katika miezi miwli iliyopita kutokana na machafuko Kaskazini Magharibi mwa nchi hiyo
-Baa la njaa lainyemelea Sudan Kusini WFP yaonya bila msaada na fedha mamilioni ya watu watakuwa hatarini
-Makala yetu leo inatupeleka zanzibar kumulika mchango wa wauguzi na wakunga

Sauti
12'3"

31 JANUARI 2020

Jaridani Januari 31, 2020 na Arnold Kayanda. Ikiwa leo ni Ijumaa utasikia Habari kwa ufupi, mada kwa kina imejikita katika mlipuko wa virusi vya corona tukiangazia nchini Kenya ambako kuna mgonjwa anayefanyiwa uchunguzi kuthibitisha iwapo ana virusi vya corona baada ya kuwasili kutoka China na dalili za homa. Na ikiwa leo ni Ijumaa tutasikia uchambuzi wa neno la wiki kutoka BAKITA.

Sauti
11'4"

30 JANUARI 2020

Jaridani Januari 30, 2020 na Flora Nducha, pata habari ikiwemo Shirika la mpango wa chakula duniani limesema uwepo wa ufadhili wa kuaminika utarahisisha uwasilishaji wa misaada. Mwakilishi wa UN wa vijana atembelea vijana kwenye kambi ya kuhifadhi wakimbizi wa ndani nchini Sudan Kusini, na nchini Niger, ujenzi wa nyumba kwa ajili ya wakimbizi na wenyeji na UNHCR na wadau ni habari njema. Makala tunaangazia mlipuko wa nzige, mashinani tupo nchini Tanzania.

Sauti
12'