Mtandao wa kukodisha baiskeli New York wafikia Milioni 10 mwaka jana
Mpango wa utekelezaji wa hatua kuhusu mabadiliko ya tabianchi, ClimateAction unaofanya kazi kwa ubia na shirika la mazingira la Umoja wa Mataifa, UNEP umezungumzia mafanikio ya mtandao wa kukodisha baiskeli kwenye jiji la New York, nchini Marekani.
Mtandao huo umemnukuu Meya wa New York, Bill de Blasio akisema kuwa kwa mwaka jana pekee mtandao huo umehudumia watu Milioni 10 kutokana na baiskeli 7,500 zinazokodishwa kwenye jiji hilo, ambapo matumizi hayo ni ongezeko kwa asilimia 24.