Nchi za Afrika ya Kati zimedhibiti vyema COVID-19-UN
Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika ukanda wa Afrika ya Kati François Louncény Fall amehutubia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na kusema kuwa harakati za serikali kwenye ukanda huo pamoja na wadau wao kukabili janga la ugonjwa wa Corona au COVID-19 zimewezesha ukanda huo kuwa wenye idadi ndogo zaidi ya wagonjwa na vifo vitokanavyo na ugonjwa huo barani Afrika.