Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António  Guteres akihutubia wakati wa kufungwa kwa mkutano wa Jukwaa la kimataifa la biashara la nchi zinazoendelea za visiwa vidogo, SIDS huko Antigua na Barbuda
UN Photo/Eskinder Debebe

Guterres atoa wito wa mageuzi katika ufadhili wa Nchi za Visiwa Vidogo Zinazoendelea

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ; António Guterres ameangazia uwezekano wa nchi za Visiwa Vidogo zinazoendelea kukabiliwa na majanga ya tabianchi na kifedha na hivyo akatoa wito wa msamaha wa madeni, mabadiliko ya taratibu za utoaji mikopo na kujumuishwa katika taasisi za fedha za kimataifa ili kusaidia nchi hizi zilizoathirika kwa kiasi kikubwa.

Sehemu kubwa ya Khan Younis imesalia magofu.
© UNOCHA/Themba Linden

Mazingira ambayo mamlaka ya Israel inawashikilia Wagaza yanatia hofu kubwa: UN

Huku kukiwa na ripoti zaidi za mashambulio ya mabomu huko Gaza usiku wa kuamkia leo Jumanne, Umoja wa Mataifa na mashirika wadau wameelezea wasiwasi wao juu ya hali ya kikatili isiyo ya kibinadamu wanakoshikiliwa na mamlaka ya Israel washukiwa wa wapiganaji wa Kipalestina katika eneo la makazi “kukiwa na madai ya unyanyasaji dhidi yao kiasi kwamba wengine walilazimika kukatwa miguu kutokana na kufungwa pingu kwa muda mrefu”.