Guterres ataka Israel na Hamas wamalize vita Gaza
Hali huko Gaza ikizidi kuwa mbaya kila uchao, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ametoa wito kwa viongozi wa Israel na Hamas wanaoshiriki mazungumzo ya kina hivi sasa, wafikie makubaliano ya kusitisha mapigano.