Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Ufunguzi wa kituo cha malezi ya watoto wachanga huko Kajiado nchini Kenya ili kuwezesha mama zao kurudi shule.
UN News

Wadau nchini Kenya waitikia wito wa Umoja wa Mataifa wa kumwezesha mtoto wa kike

Mkutano wa 68 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani, CSW68 ulifunga pazia hivi majuzi jijini New York Marekani ukipigia chepuo uwekezaji kwa wanawake na wasichana, na leo tunabisha hodi nchini Kenya wasichana waliokumbwa na ujauzito utotoni na kukatishwa ndoto za kuendelea na masomo au kupata ajira wamepata jawabu la changamoto wanazokumbana nazo pindi wakijifungua watoto wao. 

Sauti
7'35"
Katikati ya mji wa Port-au-Prince Haiti machafuko yamesababisha kundi kubwa la watu kutawanywa
© UNICEF/Herold Joseph

Hatua za kijasiri zinahitajika ili kutokomeza mateso na ukatili Haiti – UN

Ufisadi, ukwepaji sheria na ukosefu wa utawala bora uliogubikwa na viwango vya juu vya uhalifu unaofanywa na magenge, vimemomonyoa utawala wa kisheria nchini Haiti na kudhoofisha taasisi za serikali ambazo zinakaribia kusambaratika, imesema ripoti mpya ya Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu iliyochapishwa hii leo huku ikitaka hatua za haraka na za kijasiri zichukuliwe ili kukabiliana na hali ya janga inayokumba taifa hilo la Karibea.