UN yaanza uchunguzi wa mlipuko Lebanon uliojeruhi walinda amani
Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani kusini mwa Lebanon, UNIFIL, umetangaza kuwa unachunguza mlipuko uliotokea eneo la Rmeish, na kujeruhi walinda amani wanne ambao walikuwa wakifanya doria bila silaha kwenye eneo lisilo la mapigano au BLUE LINE ambalo linatenganisha Israel kutoka Lebanon na milima ya Golan inayogombaniwa na pande zote mbili.