Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Shule za Gaza zimepigwa au kuharibiwa na makombora tangu mwanzo wa vita.
© UNRWA

Mauaji Gaza lazima yakomeshwe, Türk aliambia Baraza la Haki za Binadamu

Mauaji yanayoendelea huko Gaza yamesababisha vifo vya zaidi ya watu 30,000 na lazima yakomeshwe mara moja, mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa Volker Türk ameliambia Baraza la Haki za Kibinadamu leo mjini Geneva Uswisi, baada ya karibu miezi mitano ya mashambulizi ya mara kwa mara ya Israel na kufurusha maelfu ya watu katika eneo hilo, kutokana na kuchochewa na mashambulizi ya Hamas yaliyofanyika Oktoba 7 mwaka jana.

Mapigano na ukosefu wa usalama nchini Sudan unaendelea kuwafanya watu kukimbia makwao kutafuta usalama.
© UNICEF/Proscovia Nakibuuka

Umoja wa Mataifa hauondoki Sudan – Katibu Mkuu UN

Ikiwa leo ndio siku ya mwisho ya Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kusaidia kipindi cha mpito nchini Sudan (UNITAMS), Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amesema pamoja na kwamba UNITAMS inaondoka Sudan lakini Umoja wa Mataifa hauondoki nchini humo na unaendelea kujitolea kwa dhati kutoa usaidizi wa kibinadamu wa kuokoa maisha na kusaidia watu wa Sudan katika matarajio yao ya mustakabali wenye amani na usalama.

Sauti
1'57"
Mtoto mwenye umri wa mwaka 1 anafanyiwa unchunguzi wa matibabu kama kuna dalili za utapiamlo katika kituo cha mapokezi kwenye mpaka wa Sudan na Sudan Kusini.
© WFP/Hugh Rutherford

Uongozi wa jimbo la Upper Nile nchini Sudan Kusini waomba usaidizi zaidi wa ulinzi

Huku mzozo wa Sudan ukiendelea, wakimbizi na wanaorejea wanamiminika katika mipaka ya nchi jirani ya Sudan Kusini, wengi wamekuwa wakitafuta hifadhi katika jimbo la Upper Nile nchini humo na wanahitaji msaada wa haraka wa kibinadamu.  Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini UNMISS umefanya mazungumzo na uongozi wa jimbo hilo kuona namna ya kuwasaidia.

Sauti
2'25"