UDADAVUZI: Nyenzo tano zinazohitajika kudumisha amani
Mwaka 1948, Umoja wa Mataifa ulichukua hatua muhimu kwa kupeleka askari wa kulinda amani kusaidia nchi katika safari yao ya kuelekea amani. Tangu wakati huo, zaidi ya watu milioni mbili wanajeshi, polisi na raia wamehudumu katika operesheni zaidi ya 70 za kulinda amani duniani kote, wakitoa msaada huku kukiwa na migogoro inayoendelea au matokeo ya migogoro hiyo.