Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Askari wa mpango wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani MONUSCO nchini Congo DRC akilinda wakati helkopta ya WFP ikiwasilisha msaada kwenye kambi ya wakimbizi wa ndani Ituri
© UNICEF/Diana Zeyneb Alhindawi

UDADAVUZI: Nyenzo tano zinazohitajika kudumisha amani

Mwaka 1948, Umoja wa Mataifa ulichukua hatua muhimu kwa kupeleka askari wa kulinda amani kusaidia nchi katika safari yao ya kuelekea amani. Tangu wakati huo, zaidi ya watu milioni mbili wanajeshi, polisi na raia wamehudumu katika operesheni zaidi ya 70 za kulinda amani duniani kote, wakitoa msaada huku kukiwa na migogoro inayoendelea au matokeo ya migogoro hiyo.

Mgonjwa aliye na utapiamlo mkali na upungufu wa maji mwilini katika hospitali ya mashambani kusini mwa Gaza - Aprili 24, 2024
© WHO

Sitisho endelevu la mapigano ndio jawabu la kudumu- WHO

Kutoka Geneva, Uswisi hii leo, Mwakilishi wa shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni, WHO kwenye eneo linalokaliwa la Palestina, Dkt. Rik Peeperkorn amesema wanalaani vikali shambulio la jumapili dhidi ya wakimbizi wa ndani huko Al-Mawasi linalodaiwa kusababisha vifo vya watu takribani 45.