Ntahakikisha nawainua wasanii wakike Sudan Kusini: Abul Oyay
Abul Oyay Deng Ajak ni msanii wa uchoraji anavyoinua jamii yake hususan wanawake katika taifa changa zaidi Afrika, Sudan Kusini
Abul Oyay Deng Ajak ni msanii wa uchoraji anavyoinua jamii yake hususan wanawake katika taifa changa zaidi Afrika, Sudan Kusini
Wasiwasi mkubwa wa madai ya ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu na ukatili mwingine nchini Ethiopia unapaswa kuchunguzwa na chombo cha kimataifa cha haki za binadamu, limeafiki Baraza la Haki za Kibinadamu hii leo kupitia kura maalum.
Wakati idadi ya wagonjwa wa Corona au COVID-19 wakiwa wanaongezeka tena ulimwenguni kote, wakichochewa na aina mpya ya kirusi cha Omicron, serikali nyingi zimeanza kufikiria iwapo zifunge shule kama njia mojawapo ya kupunguza kusambaa kwa maambukizi.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR limesema mapigano kati ya jamii yaliyozuka huko Kaskazini mwa Cameroon katika kipindi cha wiki mbili zilizopita yamewafurusha takriban watu 100,000 kutoka makwao, na idadi hiyo inaweza kuwa kubwa zaidi.
Tunajua kinachofanya kazi. Lakini kwa nini hatuoni athari zake tusipofanyia kazi? Ndio swali lililoongoza mazungumzo kati ya Viongozi Wakuu Wanawake wa Umoja wa Mataifa wakati wakijadili kuhusu Kukomesha Unyanyasaji dhidi ya Wanawake na Wasichana duniani.
Akijenga hoja kwamba ulimwengu "hauwezi kushinda janga kwa njia isiyoratibiwa", Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa leo Alhamis amesema kwamba nchi "lazima zichukue hatua madhubuti katika siku zijazo" kuchanja asilimia 40 ya idadi ya watu wote ulimwenguni ifikapo mwisho wa mwaka.
Shirika la afya la Umoja wa Mataifa duniani WHO leo limetangaza kwamba mlipuko wa Ebola uliozuka nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC kwenye jimbo la Kivu ya Kaskazini mwezi Oktoba ukiwa ni wa pili kwa mwaka 2021 sasa umemalizika.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF linaendesha program maalum ya lishe kwenye kaunti ya Garissa nchini Kenya kwa lengo la kunusuru maisha ya mamia ya watoto wanaosumbuliwa na utapiamlo.
Ujumbe wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini UNMISS umefanya ziara na viongozi wa dini kuwatembelea wakimbizi wa ndani walioko Nagero huko Tambura li kuweza kuwajengea matumaini lakini pia kusikiliza mahitaji yao.
Ripoti mpya ilitolewa leo na Shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni WHO kuhusu janga la COVDI-19 inaonesha matukio ya kila wiki ya visa vipya vya wagonjwa yamepungua kwa asilimia 5 na vifo vinavyohusiana na janga hilo vikipungua kwa asilimia 10 katika wiki ya kuanzia tarehe 6 mpaka 10 Desemba 2021.