Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Vurugu lazuka upya Cote d'Ivoire

Shirika la UM juu ya Ulinzi wa Amani katika Cote d’Ivoire (UNOCI) limeshtumu hali ya kuzuka tena kwa vurugu karibuni kwenye eneo la Bouake, kaskazini ya nchi. Kwa mujibu wa taarifa ya UNOCI raia wasio hatia walikamatwa, na baadhi yao waliuawa kihorera, vitendo ambavyo UM umesisitiza vinakiuka kihakika haki za binadamu. Wenye madaraka walihimizwa kuchukua hatua za haraka ili kuhakikisha jinai hii inakomeshwa haraka, uhalifu ambao UNOCI unaamini unahatarisha usalama na amani ya taifa kijumla.

Tuhuma za unyanyasaji wa kijinsia dhidi ya UM zapungua 2007 Liberia

Ripoti ya karibuni ya Shirika la UM juu ya ulinzi wa amani katika Liberia (UNMIL) imethibitisha kwamba shtumu dhidi ya wafanyakazi wa UM, ambao siku za nyuma walidaiwa kuendeleza ukandamizaji na tuhumu za unyanyasaji wa kijinsia, zimeteremka kwa asilimia 80 katika kipindi cha nusu ya pili ya mwaka 2007, tukilinganisha na kipindi hicho hicho katika 2006.