Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Vurugu lazuka upya Cote d'Ivoire

Vurugu lazuka upya Cote d'Ivoire

Shirika la UM juu ya Ulinzi wa Amani katika Cote d’Ivoire (UNOCI) limeshtumu hali ya kuzuka tena kwa vurugu karibuni kwenye eneo la Bouake, kaskazini ya nchi. Kwa mujibu wa taarifa ya UNOCI raia wasio hatia walikamatwa, na baadhi yao waliuawa kihorera, vitendo ambavyo UM umesisitiza vinakiuka kihakika haki za binadamu. Wenye madaraka walihimizwa kuchukua hatua za haraka ili kuhakikisha jinai hii inakomeshwa haraka, uhalifu ambao UNOCI unaamini unahatarisha usalama na amani ya taifa kijumla.