Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Ukraine

Jengo lililoharibiwa katikati mwa Kharkiv, Ukraine.
© UNOCHA/Matteo Minasi

Viongozi watoa maoni yao baada ya uamuzi wa Baraza Kuu la UN dhidi ya Urusi

Vita ya Ukraine ikiwa inaingia mwaka wake wa pili, wawakilishi mbalimbali wa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa wametoa maoni yao kufuatia uamuzi kwa njia ya kura uliofanywa na Kikao Maalumu cha  dharura cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kupitisha azimio jipya la kutaka amani ya haki na ya kudumu nchini Ukraine na kwamba Urusi bila masharti yoyote iondoe mara moja majeshi yake katika ardhi ya Ukraine. 

Sauti
2'22"
Jengo la kihistoria katikati mwa mji wa zamani wa Kharkiv limeharibiwa vibaya kutokana na vita nchini Ukraine.
© UNICEF/U.S. CDC/Christina Pashinka

Uharibifu wa makusudi wa utamaduni wa Ukraine lazima ukome: Wataalam wa haki za binadamu.

Takriban mwaka mmoja baada ya vita kamili kuzuka nchini Ukraine na huku kukiwa na mashambulizi mapya ya makombora yanayolenga mji wa Mashariki wa Kharkiv siku ya Jumatano wataalam wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa wametoa wito wa kukomeshwa mara moja uharibifu wa makusudi wa hazina za kitamaduni za nchi hiyo unaofanywa na vikosi vya Urusi.