Uhaba wa chanjo ya kipindupindu wasitisha mkakati wa dozi mbili- WHO
Kundi la kimataifa la kuratibu usambazaji wa chanjo nyakati za dharura, ICG limeamua kusitisha kwa muda mkakati wa utoaji wa dozi mbili za chanjo dhidi ya ugonjwa wa kipindupindu kutokana na hofu ya uwezekano wa uhaba wa chanjo hiyo.