Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Syria

Watoto wakilala katika msikiti ulioko katika wilaya ya Al-Midan ya Aleppo, Syria
© UNHCR/Hameed Maarouf

Ulinzi wa raia unasalia kuwa ndoto Syria: Tume ya uchunguzi ya UN

Ripoti mpya iliyotolewa leo na tume ya Umoja wa Mataifa ya uchunguzi nchini Syria inasema pande zote katika mzozo unaondelea nchini humo zimetekeleza ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu na ukatili katika miezi ya kuelekea tetemeko kubwa la ardhi kuwahi kushuhuduwa kwa zaidi ya karne katika ukanda huo, na kuendeleza muongo ulioghubikwa na mwenendo wa kushindwa kuwalinda raia wa Syria.

Watoto milioni 3.7 walioathirika na tetemeko Syria wanakabiliwa na zahma kubwa
UN News

Watoto milioni 3.7 walioathirika na tetemeko Syria wanakabiliwa na zahma kubwa: UNICEF

Watoto milioni 3.7 ambao walinusurika na matetemeko ya ardhi ya tarehe 6 Februari mwaka huu katika maeneo yaliyoathirika nchini Syria wanakabiliwa na ongezeko la vitisho kadhaa vya zahma kubwa, ameonya leo Mkurugenzi mtendaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto UNICEF, Catherine Russell akihitimisha ziara yake ya siku mbili nchini humo. 

Mashirika ya Umoja wa Mataifa yanasafirisha misaada kibinadamu kwa ajili ya waathirika wa tetemeko la ardhi kutoka Türkiye kwenda kaskazini magharibi mwa Syria.
© UNOCHA/Madevi Sun Suon

Ujumbe wa mashirika ya Umoja wa Mataifa watembelea walioathirika na tetemeko nchini Syria

Ujumbe wa mashirika saba ya Umoja wa Mataifa umetembelea hospitali na kliniki zinazoungwa mkono na shirika lisilo la kiserikali la Misaada na Maendeleo la Syria au SRD, Kaskazini Magharibi mwa Syria na kujionea athari za tetemeko la Ardhi lililoikumba nchi hiyo wiki mbili zilizopita pamoja na kujionea usambazaji wa misaada iliyotolewa na Umoja wa Mataifa.

Sauti
2'28"
Chakula kinasambazwa kwa watu waliokimbia makazi yao baada ya tetemeko la ardhi huko Aleppo, Syria.
© Al-Ihsan Charity

Tunataka kuwafikia waathirika wote japo kuna kikwazo cha usalama katika baadhi ya maeneo - WFP Syria

Mashirika ya Umoja wa Mataifa yanaendelea kupeleka na kusambaza misaada nchini Uturuki na Syria ili kusaidia walioathiriwa na matetemeko makubwa ya ardhi yaliyotokea Jumatatu wiki hii na kujeruhi, kuua maelfu na kuharibu miundombinu. Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) lina lengo la kuwafikia watu nusu milioni katika nchi zote mbili ijapokuwa kuna changamoto za kiusalama katika baadhi ya maeneo.

Sauti
2'59"
Watoto waliokimbia makazi yao kufuatia machafuko. Wanaishi katika kambi ya wakimbizi mipakani ya kusini magharibi mwa Syria.
© UNICEF/Alaa Al-Faqir

Mwaka mpya ukijongea, wito watolewa kuwapa matumaini watu wa Syria

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limefanya kikao cha Baraza la Usalama leo Jumatano, kuhusu hali ya Syria, ambapo limesikiliza taarifa mbili fupi kuhusu hali ya kisiasa na usalama, iliyotolewa  kwa njia ya video na Mjumbe Maalum wa Katibu Mkuu kwa Syria Geir Pedersen na Martin Griffiths Mkuu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa ya  kuratibu misaada ya dharura, OCHA.