Ulinzi wa raia unasalia kuwa ndoto Syria: Tume ya uchunguzi ya UN
Ripoti mpya iliyotolewa leo na tume ya Umoja wa Mataifa ya uchunguzi nchini Syria inasema pande zote katika mzozo unaondelea nchini humo zimetekeleza ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu na ukatili katika miezi ya kuelekea tetemeko kubwa la ardhi kuwahi kushuhuduwa kwa zaidi ya karne katika ukanda huo, na kuendeleza muongo ulioghubikwa na mwenendo wa kushindwa kuwalinda raia wa Syria.